JAFO:MSHIKAMANO WA VIONGOZI SABABU YA TANZANIA KUWA KISIMA CHA AMANI.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu Wa Rais ,Muungano na Mazingira Seleman Jafo.

........................................................

Na mwandishi wetu Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu Wa Rais ,Muungano na Mazingira Seleman Jafo amesema  nchi ya Tanzania kuendelea kuwa kisima cha Amani Duniani ni kutokana na mshikamano mkubwa wa viongozi wa Dini kuendelea kuliombea taifa.

Waziri Jafo amebainisha hayo leo Septemba 21,2021  jijini Dodoma katika kongamano la kitaifa la Amani ambalo limekwenda   sambamba na maadhmisho ya amani Duniani.

Waziri Jafo amesema  amani inaweza ikatoweka kutokana na masuala mbalimbali ikiwemo majanga ya asili ikiwemo matetemeko ya ardhi,magonjwa,uonevu,utawala usiofuata sheria na uonevu lakini Tanzania imekuwa nchi ya kuigwa kwa kustahimili amani   hivyo ni kutokana na viongozi wa dini kuwa mstari wa mbele kuliombea taifa  na kuhamasisha waumini  kutunza amani.

Hivyo,Waziri Jafo amewataka watanzania kuendelea kulinda amani kuanzia ngazi ya familia na kukemea viashiria vya uvunjifu wa amani.

Mwakilishi mkaazi ,Umoja wa mataifa[UN ],Zlatan Millisic amesema ,wao kama Umoja wa Mataifa wamekuwa mstari wa mbele kuhamasisha kama ilivyo malengo endelevu lengo namba 16  la Umoja wa Mataifa huku akipongeza serikali ya Tanzania  kwa kuendelea kulinda amani.

Nao baadhi ya wadau wa amani nchini wakiwemo wananchi na viongozi wa asasi mbalimbali za kiraia wamesema amani ni msingi muhimu kwa maendeleo ngazi ya familia mpaka Taifa.

Maadhimisho ya amani duniani huadhimishwa kila ifikapo septemba 21 ya kila mwaka ambapo mwaka huu yanakwenda sambamba na kaulimbiu isemayo,”Kujikwamua vyema Zaidi kwa ulimwengu wenye usawa endelevu. 

 

0/Post a Comment/Comments