MBARAWA AKASIRISHWA NA YANAYOENDELEA KATIKA UJENZI BARABARA YA MWENDDOKASI YA MBAGALA MISION.

Waziri  wa  Ujenzi  na  Uchukuzi  Profesa   Makame  Mbarawa (picha na mtandao)

.............................................................

NA SALYM BITCHUKA

Waziri  wa  Ujenzi  na  Uchukuzi  Profesa   Makame  Mbarawa amemtaka  mkandarasi   anayejenga  barabara  ya  mwendo  kasi   (BRT)  ya  Mbagala  Mision  kurudia  ujenzi  wa  barabara  hiyo  yenye  ukubwa  wa  kilomita  mbili  kutokana  na  kukosa  viwango  bora  vya  ujenzi.

Waziri  Mbarawa  ameyasema  hayo  leo jijini   Dar  es Salaam  akiwa  kwenye  ziara   ya   kukagua  miradi ya  barabara  za  BRT , Njia  nane  na  Kituo  cha Kipya  cha Mabasi cha  Mbagala .

Aidha  Profesa  Mbarawa  amesema  kipande  cha  barabara  ya Mbagala  Mission  kimeanza  kuonyesha  mipasuko  kabla  ya  matumimizi  kitendo  kinachoonyesha  kukosa  viwango  bora vya  ujenzi  huku  akitoa  miezi  Mitano  kwa  Mkandarasi  kuirudia   barabara  hiyo yenye  ukubwa  wa  kilomita  mbili  kwa  gharama  zake.

Aidha  waziri  Mbarawa  ameahidi  kuanza  kutumia  teknolojia  mpya  ya  kukagua  ubora  wa barabara huku  akitoa  Maelekezo  kwa  wasimamizi  wa  Barabara  nchini TANRODS  Kufika  Ofisi  za  Wizara ya Ujenzi   na Uchukuzi  kupatiwa  mtambo  utakaowezesha  kuondokana  na  barabara  sizizo  na ubora.

Kwa  upande  wake  Mtendaji  mkuu  wa  TANRODS  Mhandisi  Rogatus  Hussein  Mativila  akizungumzia  mapungufu  yaliyoonekana  katika  barabara  BRT Mbagala  amesema  yametokana  na Mkandarasi  wa  ujenzi   huo  kutumia  mchanga  usiofaa  katika  ujenzi .

Mradi  huo  wa ujenzi  wa  babarabara BRT wenye  thamani  ya Shilingi  Bilioni  217 ulianza  Desemba 10, 2018  na  ulitarajiwa  kukamilika  mwaka   huu 2021 lakini  kwa  sasa  unatarajiwa  kukamilika March  2023 kutokana  na matatizo  yaliyokuwepo awali  katika  utawala.

 

0/Post a Comment/Comments