Afisa
Mahusiano wa Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ Bank Salim Hassan akizungumza na
mwandishi wa blog hii katika katika maonesho ya wiki ya huduma za kifedha
yanayoendelea katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam
.........................
NA
MUSSA KHALID,DAR ES SALAAM
Benki
ya Watu wa Zanzibar -PBZ Bank imesema licha ya kuwahudumia wateja pia inatoa
elimu na ushauri kwa lengo la kusaidia kusogeza huduma za kifedha kwa wateja.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi katika maonesho ya wiki ya huduma za kifedha
yanayoendelea katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam Afisa
Mahusiano wa Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ Bank Salim Hassan amesema pamoja na
masuala ya elimu ya kifedha pia wanawaelimisha wateja kuweka akiba sambamba na
kufungua akaunti.
Salim
amesema benki hiyo imekuwa ikijikita kufungua matawi katika maeneo mbalimbali
ili kuhakikisha watanzania wanafikiwa na huduma za kifedha kwa ukaribu.
‘Kimantiki
hasa tupo kwa ajili ya kushirikiana na baadhi ya taasisi ambazo zinafanana na
zakwetu katika kutoa elimu ya masuala ya kifedha kwa watanzania na hapa mnazi
mmoja tunazofursa za kuwaeleza kwa undani zaidi kuhusiana na fursa zetu za
kimikopo’amesema .’amesema Salim
Aidha
Afisa Mahusiano huyo amesema ni vyema watanzani wakaitafuta pesa lakini pia kufahamu
namna ya kuitunza na kuiendeleza kwa kuwa na akauti benk.
‘Tunalenga
kuwashauri wateja wetu wafungue zile akaunti ambazo wakiziweka kwetu sisi
tutaweza kuizungusha ile pesa na faida kitakachopatikana tutaweza kukigawa
maana yake mteja wetu aweze kupata fungu kupitia huduma ya Fixed Accout’amesema
Salim
Hata hivyo amesema PBZ Benk wanaendesha katika mifumo miwili ya kihuduma ukiwemo wa kawaida pamoja na mfumo wa Kiislamu ambao hauhusishi Riba.
Post a Comment