NA MUSSA KHALID,
Taasisi ya Mifupa Muhimbili -MOI imeanza
kambi ya kufanya upasuaji wa kuondoa
uvimbe uliopo kwenye sakafu ya Ubongo kichwani ili kuwasaidia watu wenye
changamoto hiyo.
Akizungumza leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa -MOI
Dkt Respicious Boniphas amesema katika kambi hiyo madaktari wa Tanzania
wanafundishwa mbinu hiyo kutoka kwa madaktari wa Uganda ambao pia ni zao la
taasisi hiyo.
Dkt Respicious ameeleza faida ya mbinu hiyo
kuwa ni pamoja na kurahisisha muda kuwa mfupi tofauti na ilivyokuwa awali
wagonjwa walikuwa wakikaa muda mrefu wodini.
Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Upasuaji wa
Ubongo na Uti wa Mgongo Aingaya Kaale amesema kuwa takriban wagonjwa 600 sawa na wastani 30-50 kwa mwezi
ambao wamewafanyia upasuaji hivyo malengo yao ni kuwafanyia wagonjwa nane
katika wiki moja.
Ramadhan Msuya ni mmoja ya wagonjwa ambaye
anatibiwa katika Taasisi hiyo ameeleza kuwa alianza kusumbuliwa na macho lakini
wataalamu wa Afya wamemsaidia kwa kumfanyia upasuaji na hivyo kuwa katika hali
nzuri.
Hata hivyo wito umetolewa kwa watanzania kuhakikisha wanakwenda Hospitalini kufanya vipimo wanapojihisi kuumwa hasa dalili zikionyesha vichwa kuuma au macho kutokuona vizuri ili waweze kupata tiba mapema.
Post a Comment