NA MUSSA KHALID
Serikali kupitia Wizara ya Habari Mawasiliano na
teknolojia ya Habari imewahakikishia watanzania kuendelea kuweka mazingira
rafiki ya kisera na kisheria katika kuchochea na kuvutia ubunifu katika Tehama
ili kuweza kuchochea kasi katika kupambana na umaskini nchini.
Pia imewataka wanawake na wasichana wabuni katika Tehama
na kujielekeza katika matumizi ya teknolojia rahisi na rafiki ili Tehama iendeleaa
kuongeza mchangowake katika taifa.
Hayo yameelezwa jijini Dar es salaam na Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia Selestine Kakele wakati akizungumza
kwenye ufunguzi wa Kongamano la saba la
mkutano Mkuu wa Tehama ambalo limewakutanisha wataalamu mbalimbali.
Aidha amesema kuwa sera ya Tehama ambayo wanaipitia
kwa sasa ina nguzo sita ikiwa ni pamoja na miundombinu ya uchumi wa
kidigitali,usimamizi wa mazingira wezeshi,elimu ya kidigitali na uendelezaji ujuzi,ubunifu,kujenga
uchumi wa kidigitali jumuishi na huduma za kifedha za kidigitali.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tehama Dkt
Nkundwe Mwasaga amesema kuwa kongamano hilo linakwenda sambamba na kauli mbiu
isemayo Tumia teknolojia Ibukizi katika mapinduzi ya kidigitali ili kutengeneza
kazi na kuleta mafanikio kiuchumi na kijamii’
‘Katika siku ya kesho tar 17 kwenye kongamano hili tumeweka
tehama kwa vijana ikiwa inaendena na mtazamo wa kidunia katika ujumuishi wa
kuyashirikisha makundi mbalimbali ambapo tunajadili mafanikio sambamba na
kujifunza nchi za nje wao wamefanyaje kuhakikisha uchumi unakwenda vizuri”amesema
Dkt Mwasaga
Esta Mengi ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kampuni ya Tehama amesema Kongamano hilo ni moja ya hatua kubwa ambayo nchi imeifikia kwa kuweka kipaumbele katika Tehama kwa maendeleo ya jamii.
Post a Comment