Takwimu zimeonesha
kuwa mwaka 2022 vifo takribani 1,545 vimeripotiwa kwa bara la Afrika pekee
vilivyotokana na ajali za usalama barabarani huku watoto wakiwa wahanga wakubwa
wa ajali hizo, hayo ni kwa mujibu wa kikosi cha usalama barabarani cha jeshi la
polisi Nchini.
Katika kupunguza ombwe
la ajali hizo kampuni ya Puma Energy kwa kushirikiana na Amend Tanzania
wamezindua kampeni ya kuleta mabadiliko ya usalama barabarani ili kuwawezesha
watoto na kuboresha usalama wao iliyopewa jina la ‘’kuwa salama barabarani
Afrika.
Akizundua kampeni hiyo
Jijini Dar es salaam Kamishna wa jeshi la polisi CP Nsato Marijani amesema
kampeni hiyo imeunga mkono moja kwa moja jitihada za serikali katika kutokomeza
vifo vinavyotokana na ajali za barabarani.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa bodi ya Puma Tanzania Dkt selemani Majige amesema ushirikiano huo
utajipambanua katika mikao mingine ili kuweza kuwafikia watanzania wengi zaidi.
Nao baadhi ya
wanafunzi walioshiriki uzinduzi huo wamesema kuwa kampeni hiyo itawasaidia
kuepukana na ajali huku wakishahuri elimu zaidi iendelee kutolewa.
Shule tano za msingi Jijini Dar es salaam zilizotajwa kuwa na mazingira hataraishi za ajali za barabarani ni pamoja na Shule ya msingi Kibugumo, Kifuru, Msewe, Kibasila na shule ya msingi ya Mtambani.


Post a Comment