TANZANIA YASHAURIWA KUJIKITA KATIKA MATUMIZI YA GESI ASILIA.

Mkurugenzi Mtendaji wa chama cha waagizaji na wasambazaji wa mafuta Tanzania –TAOMAC wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi kuhusu hali ya biashara ya mafuta hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania imekumbwa na uhaba wa Dola.

Mkurugenzi Mtendaji wa chama cha waagizaji na wasambazaji wa mafuta Tanzania –TAOMAC akifafanua jambo kuhusu hali ya biashara ya mafuta hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania imekumbwa na uhaba wa Dola.(picha na Mussa Khalid)
.........................

NA ISSA MOHAMMED

Serikali ya Tanzania imeshauriwa kujipambanua katika matumizi ya nishati asilia ikiwemo Gesi ili kupunguza  utegemezi wa uagizaji mafuta kutoka nje ya Nchi pamoja na changamoto zingine zinazopelekea upandaji wa mafuta ya petroli na Dizeli.

Ushahuriwa huo umetolewa Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa chama cha waagizaji na wasambazaji wa mafuta Tanzania –TAOMAC wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi kuhusu hali ya biashara hiyo hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania imekumbwa na uhaba wa Dola.

Amesema hatua nyingine inayopaswa kuchukuliwa na Serikali ni pamoja na kuboresha miundominu ya kupokelea mafuta katika Bandari ya Dar es salaam ili kupunguza ombwe la kukaa muda mrefu kwa meli zinazokuja hapa Nchini kushusha mafuta hayo.

‘’Serikali inapaswa kuwa na njia za muda mrefu wa matumizi ya nishati, kwa mfano matumizi ya –CNG, hasa katika sekta ya usafiri kwahiyo itasaidia hata uagizaji wa mafuta itapungua hasa kutumia dola’’ Amesema Mgaya.

Sambamba na hilo Mgaya amesema chama hicho kimetumia euro milioni 26 katika kipindi hiki cha mwezi Aprili ili kuagiza mafuta nje ya Nchi kutokana na uhaba wa dola jambo ambalo limekua likiathiri mwenendo wa biashara hiyo.

‘’Sasa ukioanisha na dola za kimarekani zilizotumika kuagiza mzigo ambao unauzwa mwezi huu hizo Euro zilikua asilimia 25, na msambazaji unapaswa kumlipa kwa dola kutokana na mkataba ndio unatambua dola na sio Euro na hiyo inachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la bei.

Aprili 3 Mamlaka ya udhibiti wa huduma za Nishati na Maji –EWURA ilitangaza bei mpya ya mafuta ambapo kwa Jiji la Dar es salaam Petroli imepanda kutoka shilingi 3163 hadi 3257 huku Dizeli ikipanda kutoka shilingi 3126 hadi 3210 huku sababu zilizotajwa na kupanda kwa matumizi ya euro.

0/Post a Comment/Comments