MAWAKILI TANZANIA KUSHIRIKI MAFUNZO ARUSHA

*****
Na Mwandishi Wetu Dar es salaam 

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeandaa mafunzo kwa mawakili wote wa serikali nchini yatakayofanyika kwa siku tano mkoani Arusha kuanzia Machi 24 mpaka 28 ambayo yatalenga kuongeza umahiri wa utendaji kazi kwa mawakili hao ambapo Mafunzo hayo yanatarajiwa kushirikisha takribani mawakili 300.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema hayo leo Machi 19 wakati akizungumza na waandishi wa Habari kuelekea mafunzo hayo yatakayotolewa na wanasheria wabobezi kutoka ndani na nje ya nchi.

 Aamesema lengo la mafunzo ni kuboresha utendaji kazi, kutafuta mwarobaoini wa usuluhishi wa migogoro ya kibiashara, kuongeza ujuzi wa uandishi wa sheria na mchakato mzima wa kutunga sheria pamoja na kuwaelekeza mawakili hao kuwa na uzalendo na kulinda maslahi ya Taifa.

“Mafunzo haya yataendeshwa na wanasheria wabobezi wa ndani na nje ya Jamhuri wa Muungano ya Tanzania katika mada tofauti eneo la kwanza ni eneo ambalo Rais amekuwa akisisitiza kila siku katika kuimarisha uwezo wetu katika uandishi, uingiaji na majadiliano ya mikataba mbalimbali ya kimataifa au hata ile ambayo si ya kimataifa.

“Sasa nini hasa misingi ya mikataba hii na unahitaji kuwa na ujuzi gani maalumu katika meza ya majadiliano na nini ni miiko ni ipi  na vitu gani unaweza kufanya na vitu gani unaweza usifanye” amesema Johari.

Aidha ametoa wito kwa mawakili wote wa serikali ambao hawajajisajili kupata mafunzo hayo jisajili mara moja kwa kuwa yataleta tija katika sekta ya sheria.

 





0/Post a Comment/Comments