PATRICK KANUMBA NA KING KUHAMASISHA AFYA YA UZAZI KUPUTIA YOUNGAND ALIVE INITIATIVE




 Msanii Athuman Njaidi, 'Patrick Kanumba' na Gavin Kakorosa, 'King' maarufu katika tamthilia ya jua kali, na Huba wamechaguliwa katika kuhamasisha afya ya uzazi kupitia Youngand Alive Initiative kusaidia kutoa elinu kwa watoto 14 hadi 24 na vijana.


Akizungumza na waandishi wa habari, leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi

wa taasisi ya Young and Alive Initiative, Sesilia Shirima, amesema taasisi yetu ni ya vijana yenye madhumuni ya kuimarisha afya ya uzazi

kwa vijana, hasa tukilenga kuanzia umri wa miaka 15 hadi 24 wa vijana bahele.


"Taasisi yetu ilianza 2017 na wenzangu wachache tukiwa

masomoni, tulikuwa tukifanya masomo ya utabibu katika chuo cha

maafisa tabibu mkoa wa Mtwara."


Aidha aliongeza kuwa Patrick Kanumba na King in moja ya wadau ambao ni vijana watakao saidia kuamashisha vijana wenzao.


"Klabu ya afya ya uzazi ya maafisa tabibu, tuliweza kutembelea vijana

wengi Mtwara kuanzia mashuleni na kwenye jamii, tuliwafundisha namna

ya kujikinga na mimba, na maambukizi ya magonjwa ya ngono."


"Tulipo maliza masomo, tuliona haitoshi ni vyema tukaendeleza juhudi zile

huku mtaani, tukaamua kuanzisha taasisi tuliyooita young and alive

initiative, shughuli zetu nyingi zilijikita nyanda za juu kusini, mkoa wa

mbeya, songwe na njombe tukishirikiana kwa ukaribu sana na serikali za

mikoa na wilaya na kamati za afya katika kuwajengea uwezo vijana

kutambua haki zao za msingi za afya ya uzazi ikiwemo haki ya kupatiwa

taarifa sahihi za afya ya uzazi, na huduma rafiki za afya ya uzazi.


Taasisi yetu hamu yake kubwa ni kuona Tanzania yenye vijana wenye afya

na wanao tambua haki zao za afya ya uzazi, wanaweza kujikinga kutopata

mimba na kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya ngono ikiwemo

maambukizi ya virusi vya ukimwi.


Sasa leo tumekuja mbele yenu tukiwatambulisha programu yetu ya YAI

fellowship, kama tulivyo wajuza taasisi yetu inaitwa young and alive lakini

haimaanishi sisi tutakuwa young milele, na tukizeeka haimaanishi jitihada

za vijana kama hizi pia ziishe, kwa hivyo lengo la mradi wetu ni kujenga

uwezo kwa vijana kuanzia miaka 15 mpaka 24 kutambua na kuwa


viongozi katika kufikisha taarifa za afya ya uzazi kwa vijana wenzao na

huduma kwa kutumia nguzo tatu za uongozi kama utoaji huduma,

uchechemuzi na ujasiriamali jamii.

programu ya YAI fellowship, yaani mafunzo haya ya uongozi katika nguzo

hizi tatu, hayatakuwa ya mara moja tu, yatakuwa yamgawanyiko wa mara

kwa mara, kwa muda wa miezi nane.Tutakuwa tukishirikiana na wadau

mbalimbali kufanya mafunzo haya, mfano tutahusisha wadau wanaofanya

uchechemuzi, ujasiriamali jamii na utoaji huduma ili waweze kutoa ujuzi

wao kwa vijana hawa.


Serikali yetu ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania imesisitiza sana kwetu

sisi mashirika yasiyo ya kiserikali kufanyia kazi vipaumbele vinavyo

endana na vipaumbele vya nchi, hivyo basi program yetu ni sehemu ya

vipaumbele vya serikali.


Mfano mwaka huu kwa mara ya kwanza serikali

imetoa mpango wa kuimarisha afya kwa makundi ya vijana balehe,

mpango ambao ume ainisha mikakati madhubuti ya kuimarisha afya ya

kundi hili la vijana. 


Katika mpango huu vipaumbele vitatu vikubwa

vilivyowekwa inajumuisha kupunguza maambukizi ya virusi ya UKIMWI

kwa vijana, kupunguza mimba za utotoni na kupunguza ukatili wa kijinsia.


Ukiangalia vipaumbele hivi vitatu vikubwa vyote vinalenga eneo la afya ya

uzazi na hivyo jitihada za kuhakikisha mpango huu unatimia zinatuhitaji

sisi vijana.Ukiachilia mpango huu bado kuna sera zingine kama vile

mpango wa kumaliza ukatili wa kijinsia na sera ya vijana ya taifa.

0/Post a Comment/Comments