SILAHA HARAMU 5230 ZA TEKETEZWA NA JESHI LA POLISI

 






                ************************


Waziri wa Mambo Ya Ndani George Simbachawene ameongoza  zoezi la kuteketeza silaha 5230  ambazo zimekusanywa  kwa kipindi cha mwaka  2018 hadi October 2021ambazo zimepatika kwenye matukio mbalimbali ya kiuhalifu.



Akizungumza  leo katika zoezi  la uteketezaji wa silaha hizo a katika viwanja vya  Shabaha jijini Dar-es-salaaam, amesema   serikali itaendele kutoa ada za michango ya  mwaka ili kuiwezesha sekretalieti  kufanya majukumu yake kikamilifu.



"Tukiwa tunafunga maadhimisho ya siku  16 za kupinga ukatili wa kijinsia nikumbushe tuu silaha zimekuwa zikitumika katika  kutekeleza ukatili wa kinjinsia  hivyo tunapaswa kuzifichua ili kukomesha ukatili huu ,serikali ya Tanzania itahakikisha kuww  inasimamia hali ya usalama wa nchi na watu wake". amsema waziri simbachawene.



Waziri amesema analipongeza jeshi la polisi na vyombo vingine vya ulinzi na  usalama kwa kufanikiwa kukamata  silaha ambazo zilikuwa katika mikono ya wahalifu.



Nae Mkuu wa jeshi la Polisi Simon sirro amesema takwimu za silaha ambazo zinateketezwa  leo  kwa kipindi cha mwaka 2018 mapaka oktoba 2021 ni  Magobole 3724, Rifle 573, pisto 20, G3 1, AK47 111, ASR 5 , shourtgun  789, FA 7. 



Kwa upande wa Kamshina Msaidizi wa Polisi na Mkuu wa kitengo cha uthibiti  wa silaha  Renada Milanzi amesema kauli mbiu na la zoezi hili ni Fichua silaha haramu kwa maendeleo endelevu ya Nchi.



"Silaha 5230 zimepatika kwenye matukio mbalimbali katika operation ya kuondoa silaha haramu katika nchi yetu, kesi mbalimbali amabzo mahakamani zimetoa uhamuzi wa kutahifisha silaha kutoka kwa wamiliki ambao wamekeuka sheria ya umiliki wa silaha ya 2015"Amesema Renada



Aidha amesema  tukio hili litafanyika kwa Makubaliano mbalimbali ya kimataifa na Makubaliano ya umoja wa Afrika.



Kwa upande Mkuu wa  mkoa Amos makala amesema zoezi hili litawajenga wananchi uelewa kuhusiana na silaha haramu na kuwaomba wananchi kutoa taarifa kw jeshi la polisi pale  pale wanapo baini mtu ambae anatumia silaha kinyume cha sheria.

0/Post a Comment/Comments