MBATIA ;NDUGAI BADO NI SPIKA WA BUNGE KWA MUJIBU WA KATIBA

Mwenyekiti wa Chama cha siasa cha NCCR Mageuzi James Mbatia amesema Job Ndugai bado ni Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Mbatia ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wanahabari ikiwa ni siku moja baada ya Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai kuandika barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM akisema kuwa alipaswa kuandika barua hiyo kwenda kwa Katibu wa Bunge.

Mwenyekiti huyo amesema mambo yote yanayoendelea kwa sasa nchini bado ni Afya kwa taifa kutokana na watanzania wanaendelea kuyajadili hoja ya usalama wa Taifa hivyo ni vyema yasichukuliwe hasi ili taifa lisiweze kuparanganyika.

Aidha amesema utaratibu wa Namna Spika kujiuzulu uko kwenye katika ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 149(1)(c) kuwa iwapo mtu huyo ni spika au Naibu Spika wa Bunge basi taarifa hiyo ya kujiuzulu iwasilishwe kwenye Bunge hivyo ameeleza migongano inayoendelea ni vyema ikasimamiwa ili taifa liwe kwenye usalama.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo amewashauri viongozi na wadau mbalimbali wakiwemo wastaafua kuandaa meza ya mazungumzo ili kujadili yanayoendelea nchini.

0/Post a Comment/Comments