NLD YATANGAZA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KATIKA MIKOA 10

Chama cha NLD kimesema kitashiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika mikoa 10 nchini, huku kikipongeza mchakato wa uchaguzi huo kwa kusema kuwa unaenda vizuri na umekuwa ni wa ushirikishwaji.

Akizungumza na waandishi wa habari Katibu Mkuu wa NLD Doyo Hassan Doyo amesema mchakato wa uchaguzi umekuwa wa haki na unakwenda na majadiliano ambapo vyama vyote 19 vilishiriki mkutano ulioandaliwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Doyo amesema ni hatua kubwa katika siasa za nchi kwa kuwa hakuna chama hata kimoja kilichosema hakitashiriki uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27,2024.


 

0/Post a Comment/Comments