*****
Na Ester Maile....Dodoma
Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Bunda ya wanufaisha wakazi 195,848 mawka2024 kati ya hao Asilimia 85 yenye sawa na wakazi 165613 wapata huduma ya maji ya bomba Kwa kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Dkt samia Suluhu Hassan.
Ameeleza hayo Mkurugenzi mtendaji Esther Gilyoma wakati akizungumza na waandishi wa habari leo 6 march 2025 jijini Dodoma akieleza mafanikio katika mamlaka hyo.
Gilyoma amesema chanzo cha maji hayo ni ziwa vikitoria ambapo kuna umbali wa kilomita 24.8 kutoka katika kijiji cha Nyabehu na uzalishwaji wake ni wastani wa mita za ujazo 2976m3 kwa siku.
Pamoja na kupambana na usafi wa mazingira kwa sasa Mamlaka ya maji safi Bunda inaujenzi wa mradi wa miundombinu ya majitaka katika eneo la Butakale ,kwa ajili ya usafi wa mazingira na mradi utakamika ndani ya mwaka huu wa fedha 2024/2025.
Vile vile Mwenyekiti wa bodi ya maji safi bunda Jushua chacha Merumbe, ameeleza kuwa hali iliyopo sasa hivi bunda ni bora kuliku hapo awali pia amesema kwa kata 13 zilizopatiwa maji zinaendelea kutumia na kufurahia huduma hyo ambayo awali ilikuwa ni changamoto kwa bunda.

Post a Comment