EQUITY NA SERIKALI WAJIPANGA KUIMARISHA UCHUMI KUPITIA UWEKEZAJI


Serikali imesema itaendelea kuchukua mwelekeo wa kimkakati wa kuwekeza kwenye maeneo yenye uwezo wa kukuza uchumi jumuishi na shindani, ambapo kipaumbele kimewekwa katika sekta ya usafiri ili kurahisisha biashara, kuvutia uwekezaji wa ndani na nje, pamoja na kuwaunganisha wazalishaji na masoko, hatua inayolenga kuharakisha maendeleo ya taifa kwa njia endelevu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara Suleiman Jaffo, wakati wa maonesho ya kibiashara yaliyoandaliwa na Equity Bank Tanzania, Mkuu wa Chuo cha CBE, Profesa Tandi Luoga amesema fursa zilizopo katika sekta ya utalii hazipaswi kupuuzwa,amesisitiza kuwa kutumia vyema urithi wa asili na tamaduni za taifa kunaweza kuifanya Tanzania kuwa kivutio kikuu cha utalii na eneo lenye fursa pana za uwekezaji katika malazi, usafiri na huduma za kijamii.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Equity Bank Tanzania, Isabela Maganga amesema mkutano huo umeleta pamoja wawekezaji na wafanyabiashara kutoka zaidi ya nchi 15, huku wajumbe zaidi ya 230 kutoka Afrika, Ulaya, Asia na Mashariki ya Kati wakijisajili kushiriki,na amesema benki yao iko tayari kuunga mkono safari ya uwekezaji nchini kwa kuunganisha wadau, kuwezesha mitaji, na kuinua biashara zinazomilikiwa na wanawake na vijana, ikiwa ni sehemu ya kuchochea ukuaji wa uchumi jumuia.

Naye Mkurugenzi wa chemba ya wafanyabiashara wenye viwanda na kilimo Oscar Kisanga amesema kuwa mikutano kama hiyo ni muhimu kwa wafanyabiashara kwani unatoa nafasi kwao kupata fursa katika soko huru la Afrika ambalo wafanyabiashara wanatakiwa wajiandae na kuzalisha bidhaa zitakazokubalika.








 

0/Post a Comment/Comments