Rais wa Jamhuri ya Namibia Dkt Netumbo
Nandi-Ndaitwah anatarajiwa kufanya ziara ya Kiserikali ya siku mbili nchini
Tanzania kuanzia kesho tar 20 hadi 21 Mei mwaka huu kwa mwaliko wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluh Hassan.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Naibu Mkurugenzi
wa Mawasiliano ya Rais,Ikulu Shaaban Kissu imeeleza kuwa Ziara hiyo ya kwanza
ya Rais Dkt Nandi-Ndaitwah chini Tanzania tangu aapishwe kuwa Rais wa Jamhuri
ya Namibia tar 21 Machi,2025 na inalenga kukuza ushirikiano wa kisiasa,kiuchumi
na kijamii ikiwemo katika nyanja za biashara,uwekezaji na elimu.
Tanzania na Namibia zimejenga uhusiano wa muda mrefu
wa kidugu na kidiplomasia,hivyo ziara hiyo itafungua fursa mpya za ushirikiano
zitakazowawezesha wananchi wan chi zote mbili kunufaika kiuchumi
Post a Comment