
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ACP Muliro Jumanne,
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linamshikilia Grace Mushi miaka 25 kwa tuhuma za kumchoma moto ndani ya nyumba aliyekuwa mpenzi wake, Khamis Abdallaah miaka 25.
Akizungumza
leo Dar es salaam Kamanda wa Kanda hiyo, Jumanne Muliro amesema kuwa tukio hilo lilitokea Julai 16 saa nane usiku
maeneo ya kwa Mzungu Mbezi Makabe katika Wilaya ya Ubungo.
Kamanda
amesema kuwa Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni
mgogoro wa kimapenzi.
Post a Comment