Naibu Waziri wa TAMISEMI na mbunge wa jimbo la Tunduma David Silinde amewaagiza mwenyekiti wa ujenzi wa kituo cha Afya cha Chiwezi Eddy Mwelela na Msimamizi wa ujenzi huo Michael Masai kuandika baraua kwenda ofisi ya Rais TAMISEMI kueleza sababu ya matumizi makubwa ya mwanzo ya ujenzi katika hatua za msingi ambapo imetumika zaidi milion 80 huku nguvu kubwa ikiwa imetoka ya wananchi kuchimba msingi,kubeba mawe,mchanga.
Hatua hiyo imekuja baada ya ukaguzi wa Naibu waziri Silinde katika kata ya Chiwezi kukagua miradi ya maendeleo na kukuta fedha kiasi kikubw acha fedha kimetumika tofauti na uhalisia wa gharama za vitu vilivyopo hali ambayo imempa wasiwasi wa matumizi mabaya ya fedha na kutaka maelezo ya fedha hizo zimetumikaje na kutaka watumishi wanaosimamia miradi wasimjaribu kukwamisha miradi hiyo kwasababu ipo kijijini basi ubadhilifu ufanyike na kutaka mpaka ikifika mwezi wa tisa akute ujenzi umefika mbali kabla hajachukua hatua kali za kinidhamu.
"Ujenzi wa mradi huu wa kituo cha Afya ni mkombozi wa wananchi wa kata hii ya Chiwezi ambao walikuwa wanatembea umbali mrefu wa zaidi ya kilometer 25 na wakati wa mvua hushindikana kusafiri kabisa kutokana na ubovu wa barabara na kusababisha baadhi ya vifo vya wajawazito au watoto wanaochelewa kupata huduma wanazo zifata kituo cha afya Tunduma hivyo watendaji msinijaribu kuchezea fedha hizo"Silinde.
Kwa upande wao Diwani wa Kata ya Chiwezi Francis Sikanyika na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Momba Twaha maulidi wamemshukuru Rais Mama Samia Suluhu kuwapa fedha za ujenzi huo na kuomba wataalam wasimamie vizuri ujenzi ili wananchi wapate huduma nzuri
Wakijitetea kwa Naibu waziri Silinde mwenyekiti wa ujenzi wa kituo cha Afua Eddy Mwelela na Msimamizi wa ujenzi Michael masai walisema wametumia kiasi hicho kwa kuchimba Kisima amcho kimetumia milion 24 na kununua siment tani 60 na vifaa vingine ambavyo gharama yake imekuja milion 81 na kwasasa wamebakiw ana milion 400 na zaidi katika milioni mitano walizopewa kwa ajili ya ujenzi
huo

Post a Comment