RAIS ANUSURIKA KUUAWA KWA KISU MSIKITINI

 


Wanaume wawili wamejaribu kumchoma kisu rais wa mpito wa Mali, Assimi Goïta katika msikiti uliopo katika Mji Mkuu, Bamako.

Kanali Goïta allikuwa akihudhuria ibada ya siku ya Eid ul-Adha katika msikiti wa Grand Mosque.


Mafisa wanasema washambuliaji, ambao kwa mujibu wa Shirika la Habari la AFP walikuwa ni wawili, wamekamatwa na rais ameondolewa kwenye msikiti huo kwa usalama wake.


Haijafahamika iwapo Kanali Goïta, ambaye aliongoza jeshi kuchukua mamlaka mwezi Agosti, alijeruhiwa.


Waziri wa masuala ya kidini Mamadou Kone aliliambia shirika la AFP kwamba mwanaume ali "jaribu kumuua rais wa kisu".


Mkurugenzi wa msikiti aliliambia shirika la habari kwamba mtu alimlenga waziri lakini alimjeruhi mtu mwingine.


Kabla ya mapinduzi ya mwezi Agosti nchi hiyo ilikuwa inakabiliwa na maadamano juu ya ufisadi na waasi wa Kiislam walikuwa wameyateka maeneo mengi ya nchi.


Kanali Goïta aliingilia kati tena mwezi Mei, akachukua nafasi ya serikali ya mpito na kuchukua mamlaka kama rais- aliahidi kukabidhi utawala wa kiraia mamlaka kama ilivyopangwa mwaka ujao.



0/Post a Comment/Comments