...................................
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi Cha
Shilingi Milioni 100 kwa ajili ya Ujenzi wa Paa la Kisasa la kuzuia Jua na Mvua
kwa Wahanga 1,800 wa Soko la Kariakoo waliohamishiwa Machinga Complex.
Mkuu wa Mkoa wa
Dar es salaam Amos Makalla amezungumza na wafanyabiashara hao jijini Dar es salaam na kuthibitisha kupokea
fedha hizo ambapo amesema baada ya Jana kuwatembelea na kuwasikiliza, Rais
Samia ameona changamoto hiyo na hivyo ametoa Milioni 100 ili lijengwe Paa la
Kudumu kwa Bati la Kisasa.
RC Makalla
amewaelekeza Suma JKT ambao ndio wajenzi kuanza Ujenzi Mara moja ili
Wafanyabiashara hao wafanye biashara bila kero.
Kuhusu suala la Meza, RC Makalla
amesema tayari amepatikana Mkandarasi atakaejenga Meza za kisasa za kuhamishika
kuendana na hadhi ya Soko.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa ameelekeza Viongozi wa Jiji la Ilala kuhakikisha wanaboresha miundombinu ya Taka, Mifumo ya Maji, Mifumo ya umeme na wafunge Vizima Moto ili kukabiliana na majanga ya Moto.


Post a Comment