RC ARUSHA AWATAKA WANANCHI KUEPUKA MIKUSANYIKO



Na Abel Paul-Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh.John Mongela amewataka wananchi wa Mkoa wa Arusha kuachana na mikusanyiko isiyo ya halali na kutumia barakoa kunawa  maji tililika kujikinga na ugonjwa wa korona, ambao unasumbua dunia katika kipindi hiki.
 
Ametoa kauli hiyo jana Julai 22/2021 katika ziara yake na wadau wa kilimo cha matunda, mboga mboga, na kilimo cha maua(TAHA) katika wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha.

Kwa upanda wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP-JUSTINE MASEJO  amesema "Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limepokea maelekezo hayo ya serikali ngazi ya Mkoa kwa wale wote watakao fanya mikusanyiko isiyo  halali,  hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao".

0/Post a Comment/Comments