RC MAKALLA AKERWA NA FAINI ZA MAEGESHO YA MAGARI


Asema watekelezaji hawana weledi na kusababisha kero na taharuki.


Aitisha kikao Cha dharuracha Wakurugenzi na TARURA kujadili.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla ameonyesha kukasirishwa na *utaratibu usiofaa wa ukamataji wa magari* kwenye maegesho yasiyo rasmi *"wrong parking"* ambapo ameelekeza kuhitishwa kikao Cha pamoja baina yake, *Wakurugenzi wa Halmashauri na TARURA* ili kupatia ufumbuzi Jambo hilo.


*RC Makalla* amefikia hatua hiyo baada ya kupokea *Malalamiko* mengi ya Wananchi juu ya *utaratibu mbovu* unaotumika na kusema Kama kiongozi *hawezi kuruhusu Jambo hilo liendelee.*


Aidha *RC Makalla* amesema amebaini  pia baadhi ya *vijana wanaofanya kazi hiyo wamekosa weledi na busara* na wengi wao wamekuwa *wakivizia* mtu afanye kosa ili wamuadhibu badala ya *kutoa elimu* ili makosa yasifanyike.


*Mheshimiwa Makalla* amesema hayo wakati wa uwekaji wa *Jiwe la Msingi kwenye Jengo la utawala la Manispaa ya Ubungo* ambapo ameipongeza Manispaa hiyo kwa *usimamizi mzuri wa fedha za Serikali na kuwataka Watumishi kutoa huduma Bora kwa wabanchi.*


Hata hivyo *RC Makalla* ameipongeza Manispaa hiyo kwa *ukusanyaji Mapato* Jambo linalopelekea waanze *kutekeleza miradi kwa Fedha za ndani* na pia kutumia *Force akaunti* kukamilisha miradi iliyokuwa ikisuasua ikiwemo Jengo hilo la utawala.

0/Post a Comment/Comments