Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
Mazingira Clara Makenya akizungumza katika kikao cha wadau wa chakula leo jijini Dar es salaam
Mbunge wa Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro Saasisha Mafuwe akizungumza katika kikao cha wadau wa chakula
Mkurugenzi Idara ya usalama na Chakula Wizara ya Kilimo Dkt Honest
Kessy akizungumza katika kikao hicho cha wadau wa chakula jijini Dar es salaam
NA MUSSA KHALID DAR ES SALAAM
Serikali imeshauriwa kufanya mapitio ya sera miongozo ya uzalishaji, na kuongeza jitihada za kuelimisha jamii hasa masuala ya Uwekezaji wa Kilimo ili kusaidia kuepukana na janga la uhaba wa chakula Nchini itayosababisha njaaa kwa jamii.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam Dar es salaam na Mwenyekiti wa kikundi cha Wabunge Vinara wa usalama wa chakula –Food Safety Mbunge wa viti maalum Neema Lugangira katika Ufungunguzi wa kikao cha wadau wa chakula ambapo amesema serikali haina budi kuboresha mifumo ya chakula kuanzia kwa wazalishaji,watunzaji kwenye maghala na walaji kwani chakula lazima kiangaliwe ili Afya ziwe bora.
Lugangira amesema Nchi ya Tanzania bado baadhi ya maeneo yanakabiliwa na uhaba wa chakula hivyo kusababisha watoto kuwa na udumavu katika ukuaji wao na utapiamlo kutokana na vyakula wanavyokula.
Naye Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Mazingira Clara Makenya amesema Kilimo cha sasa kimekuwa kikiathiri mazingira kutokana na wakulima kutumia madawa na viuatilifu hali inayopelekea siku hadi siku ardhi kupoteza mbolea yake ya asili na hivyo mazingira kuharibika na kusababisha uzalishaji ukipungua.
Kwa upande wake Mkurugenzi Idara ya usalama na Chakula Wizara ya Kilimo Dkt Honest Kessy amesema katika suala la uzalishaji bado limekuwa na changamoto kutokana na tija kuwa chini.
Saasisha Mafuwe ni Mbunge wa Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro amesema lengo lao ni kujadili na namna ya watanzania wanaweza kupata chakula chenye virutubisho vinavyohitajika ili kuweza kuondoa udumavu kwa watanzania.
Hata
hivyo imeelezwa kuwa kupitia kikao hicho
na Mkutano Mkuu wa Chakula unaotararajiwa kufanyika Septemba mwaka huu New York
Nchini Marekani wawakilishi watakaokwenda watakuja na suluhisho .



Post a Comment