Shekh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Alhad Mussa Salim alipozungumza na waandishi wa habari leo Ofisini kwake jijini Dar es salaam.
NA MUSSA KHALID DAR ES SALAAM
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni
rasmi katika swala ya Sikukuu ya Eid-il-Adhwha itakayofanyika
kitaifa kwenye msikiti wa Mtoro jijini Dar es salaam July 21 mwaka huu.
Akitoa
taarifa hiyo leo jijini Dar es salaam Shekh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Alhad
Mussa Salim amesema sikukuu hiyo ya Eid-il-Adhwha au Idd El Hajj itaambatana
na baraza la Idd kwa lengo la kuwaelimisha waumini wa Dini ya Kiislamu
kuhusiana na sikukuu hiyo kutoka kwa viongozi wao.
Shekh
Alhad amewakumbusha waislamu kuwa ibada kubwa kwa siku hiyo ni kuchinja mnyama
ikitokana na tukio la kihistoria ambalo Nabii Ibrahim alipotaka kumchinja
mwanawe Ismail baada kuota ndoto akimchinja.
‘Ile
siku ya Iddi ndio siku ya kuchinja hivyo waislamu tunatakiwa tuchinje kwani ni
ibada kongwe tukikumbuka tukio la Nabii Ibrahim alipomuambia mwanawe baada ya
kuona ndoto na tukumbuke ndoto za mitume ni ujumbe hivyo alimuambia mwanawe
ameona amchinje na hivyo Ismail akawa tayari kuchinjwa na baba yake kilichotokea
baada ya hapo Mwenyezimungu alimfidia Ismail kwa kichinjo kitukufu kwa
kupelekwa kondoo maalum achinjwe badala ya ismail hivyo jambo ambalo mpaka leo
tumekuwa tukichinja’amesema Shekh Alhadi
“Swala hii ni swala ya kimataifa na sisi
waislamu wa Dar es salaam tumepewa heshima hiyo kuwa ndio wenyeji wa shughuli
za wala hiyo kwa mwaka huu hivyo niwakumbushe waislamu wote kuhakikisha
munajitokeza kwa wingi kuswali swala hiyo’amesema Shekh Alhad
Hata
hivyo Shekh huyo wa Mkoa wa Dar es salaam ametoa tahadhari kwa wenye kuchinja
kuangalia na kuwachagua wanyama ambao hawana aibu yeyote ikiwemo wenye
ulemavu kama chongo,waliokatwa sikio pamoja na kukatwa mkia bali wamchinjie
mola wao myama aliyemzuri.
Katika hatua nyingine Shekh Alhad ametumia fursa hiyo kuwataka waumini wa Kiislamu kuchukua tahadhari mbalimbali za kukabiliana na ugonjwa wa Uviko-19 ikiwa ni pamoja na kutopeana mikono kwani ni jambo litakalosaidia swala hiyo kuswaliwa bila yakuwa na athari yeyote.


Post a Comment