BARAZA LA MADIWANI JIJI LA DAR LASITISHWA BAADA YA KUKOSEKANA MENEJA WA TARURA..

Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam na Mwenyekiti wa Baraza hilo,Omari Kumbilamoto akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani

Kaimu Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Tabu Shaibu akizungumza na waandishi wa habari akitolea ufafanuzi kuhusu suala la TARURA

....................................................

NA MUSSA KHALID DAR ES SALAAM

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam limelazimika kusitisha kikao cha baraza hilo baada ya Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kukosekana katika kikao hicho.

Hayo yamejiri leo jijini Dar es salaam katika kikao cha kawaida cha baraza hilo kwa lengo la kupitia taarifa za utendaji kazi wa jiji cha Robo ya nne ya mwaka.

Akizungumza katika Kikao hicho Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam na Mwenyekiti wa Baraza hilo,Omari Kumbilamoto amesema TARURA wametenga takriban Bill 10 kwa ajili ya ujenzi wa barabara katika mkoa wa Dar es salaam lakini kuna baadhi ya Kata barabara hazijajengwa.

‘Changamoto kubwa na masikitiko ni kwamba TARURA kabla hawajatenga hizi fedha walitembelea kata zote 36 wakakutana na madiwani na maafisa watendaji na serikali za mitaa na wakawauliza madiwani kuwa ni kipaumbele kipi za barabara kwenye mitaa yao na cha kustaajabisha na masikitiko kuna kata kama ya Chanika haijawekewa hata barabara moja’amesema Meya Kumbilamoto

Aidha Meya Kumbilamoto amesema kama inavyoelewaka kwa sasa madiwani hawahusiki na matengenezo ya Barabara kwani zote zipo chini ya TARURA.

Katika hatua nyingine Meya Kumbilamoto amesema wameadhimia walitenga kwenye bajeti yao takriban Bill 2 kujenga madarasa 200 ya shule za sekondari hivyo amemuelekeza Mkurugenzi kuwa hawatasubiri mpaka watoto wafaulu bali waanze mgawanyo wa fedha mapema.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Tabu Shaibu amesema katika Maazimio ya nyuma waliadhimia na walikubaliana TARURA waweze kubainisha mapungufu na jambo lolote linalohusiana na barabara.

Hata hivyo Baraza hizo limeadhimia kuafanya kikao kingine baada ya shughuli za upokeaji wa mwenge Agost 18 mwaka huu.

0/Post a Comment/Comments