Msajili wa
Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi wakati alipokutana na kuzungumza na
safu mpya ya uongozi wa baraza la Vyama vya siasa nchni (picha na mtandao)NA MUSSA KHALID DAR ES SALAAM
Baraza la Vyama vya siasa nchini limetakiwa kuepukana na mvutano kati ya baraza hilo na baraza la kituo cha demokrasia TCD kwani wote kwa Pamoja wana jukumu la kukuza demokrasia Nchini
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi wakati alipokutana na kuzungumza na safu mpya ya uongozi wa baraza hilo baada ya uongozi huo kupatikana katika uchaguzi uliofanyika julai 28 2021 Jijini Dodoma
Jaji Mutungi
amelikumbusha baraza hilo kuhakikisha linakuwa na mikakati ya kukuza
demokrasi na utawala bora ili kuendelea
kukuza amani ya nchi.
Aidha
Jaji Mutungi amesema baraza linawajibu
wa kuwaaminisha watanzania kwa vitendo juu ya dhana na uwepo wa
demokrasia na utawala bora Nchini na
siyo kuwa na mvutano na baraza la kituo cha demokrasia TCD.
Juma Khatibu ni Mwenyekiti wa Chama Cha siasa Cha Ada Tadea Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya siasa,amesema Baraza hilo litaendelea kufanya siasa za kistarabu ikiwa ni pamoja na kuweka uzalendo mbele wa taifa ili kufanikisha maendeleo ya nchi na kuahidi kuendeleza jitihada za kuwa kiungo bora kati yao na Seikali.
Baraza
hilo jipya ya vyama vya siasa pia limezindua kamati ya uongozi ambayo itaanza
kazi mara moja ya ujenzi wa Demokrasia na utawala bora nchini.
Post a Comment