POLISI DAR YAKAMATA WATU 13 KWA MADAI YA KUFANYA UTAPELI.

 

Jeshi  la  Polisi  kanda  Maluum   ya  Dar es Salaam limefanikiwa  kuwakamata  watu  13 wa makosa ya kujipatia pesa kwa njia za udanganyifu (utapeli) wa madini bandia.

Akitoa  taarifa  hizo  kwa  waandishi  wa  habari  leo  jijini  Dar  es Salaam Kamanda  wa  Polisi  wa Kanda Maalum  ya  Polisi ACP    Muliro  Jumanne Muliro  amesema   watuhumiwa  hao  wamekamatwa  katika  operasheni  kali  inayoongozwa  na taarifa fiche inayolenga kuzuia vitendo vya  kihalifu na kuwakamata wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Kamanda  Muliro amesema   watuhumiwa  hao  wamekamatwa  Augusti  20 2021 katika maeneo  ya  Mbezi  Makonde  Wilayani  Kinondoni huku  akiwataja  watuhumiwa  hao   wakiongozwa  na Christopher Robert@Mayanga,(29),Mkazi wa Tabata Bima, Harold Martin@Pouwes,(60) raia Afrika Kusini na wenzao kumi  na moja kwa tuhuma  za  uuzaji wa madini bandia.

Aidha  Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limeyakamata  na  kuyachunguza magari hayo 6, ambayo yalikuwa  yakitumiwa  na  watuhumiwa  hao  amabayo  ni  gari  namba  T 479 Dhw Toyota Prado, T  740 Dsw  Toyota  Alphard,   T 273 Dhm Toyota Noah,  T 241 Dvu Mercdes Benz,  T 751 Dk Toyota Racts Na T 974 Dmr Toyota Brevis.

Katika  tukio la pili, Jeshi  la  polisi  Kanda  Maalum  ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwakamata watu wanne kwa tuhuma za kutenda makosa ya unyang’anyi wa kutumia nguvu na kuiba / kupora  pikipiki toka kwa waendesha pikipiki  maarufu bodaboda.

Amewataja  watuhumiwa  hao  kuwa  ni  Hizza Herbert (52), Mkazi Tabata, Richard George (45), Mkazi wa Buguruni , Arif Henry (21), Mkazi wa Buguruni, Saad Mohamed (25), Mkazi wa Mburahati.

Tayari  Baadhi ya pikipiki hizo zimeshatambuliwa na wamiliki halali  huku  Watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

0/Post a Comment/Comments