Mkuu wa Idara ya Program inayoendesha Program ya Museam Arts Explosion kutoka Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni bw.Chance Adam Ezekiel akizungumza kuhusiana na Program ya Museam Arts Explosion ambayo hufanyika kila ijumaa ya mwisho wa mwezi.
NA MUSSA KHALID DAR ES SALAAM
Watanzania
wametakiwa kupenda kutembelea kwenye vivutio vya utalii vilivyobeba urithi wa nchi
ili kufahamu historia yake ilipotoka na inapokwenda na ilipo.
Hayo
yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa Idara ya Program inayoendesha Program ya Museam Arts Explosion kutoka Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Chance Adam Ezekiel wakati akizungumza na mwandishi wa
habari hii akieleza kuhusiana na Program ya Museam Arts Explosion ambayo
hufanyika kila ijumaa ya mwisho wa mwezi.
Chance
amesema pindi mtu akitaka kujua urithi wa nchi ni vyema akatembelea maeneo
mbalimbali ya makumbusho pamoja na malikale zilizopo nchini kwani ndimo
historia za nchi zimeandikwa.
‘Imekuwa
ni changamoto kwa wanafunzi wengi wanaosoma masomo ya historia hawatembei
kujifunza kwa nadharia na vitendo bali wanakariri jambo ambalo wanashindwa kuwa
na uelewa mkubwa’amesema Chanche
Awali
Mkuu huyo wa Idara ya Program ya Museam
Arts Explosion akieleza kuhusiana program hiyo,amesema malengo yao ni
kuhakikisha wanainua na kukuza vipaji vya vijana wa kitanzania waweze kuufahamu
urithi wa utamaduni kupitia sanaa zao.
‘Sisi
tuna shughulika zaidi na wale wasanii wadodo na wanaochipukia kwa kuwakutanisha
katika jukwaa moja na wanafanya maonyesho ambapo tangu mwaka 2016 tumefanya na
wasanii wengi sana na hicyo wamejipatia mafanikio kwani tunaaalika watu wengi
wakiwemo mabalozi na kutoka serikalini’ameendelea kusisitiza
Michael
James ni Muandaaji wa Mchezo wa jukwaani wa Zama amesema lengo la kufanya
mchezo huo ni kuwaelimisha watanzania ili waweze kuachana na tamaduni za kale
zilizopitwa na wakati zinaikandamiza jamii ya kitanzania.
Hata
hivyo vijana wametakiwa kuepuka kuiga maadili ya nje ya nchi badala yake wafate
na kupenda kuishi kulingana na maadili ya kitanzania ili kuendelea kukuza
utamaduni wao.


Post a Comment