NA
MUSSA KHALID DAR ES SALAAM
Imeelezwa kuwa Taasisi za haki za Binadamu
zikizingatia misingi ya kikatiba na kisheria na haki za binadamu zitasaidia
kulinda haki hizo na kuondoa changamoto kwa jamii.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam
na Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania
(THRDC) Onesmo Olengurumwa wakati akizungumza katika Mkutano
na mafunzo ya siku tatu inayohusisha Mtandao wa Taasisi za haki za Binadamu
Afrika wakijadili azimio la Marakeshi ambalo limeweka utaratibu mzuri wa
kulinda haki za binadamu.
Olengurumwa
amesema kwa mujibu wa katiba na sheria za kimataifa mwenye jukumu la kulinda
haki za binadamu ni serikali pamoja na taasisi zake zikiwemo Mahakama pamoja na
Polisi.
‘Tunafahamu
kwamba ulinzi wa haki za binadamu mwenye
jukumu la kwanza la kulinda haki hizo kwa mujibu wa katiba na sheria za
kimataifa ni serikali zetu na taasisi zake na ndio maana tuna polisi’amesema
Olengurumwa
Aidha
Mratibu huyo amesema ni vyema haki za binadamu zikaendelea kuheshimiwa ili
ziweze kusaidia kuitetea jamii katika changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo.
Kwa
upande wake Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu Mohamed Hamis Hamad
amesema ili kuzilinda haki za binadamu pasavyo ni vyema taasisi za kiserikali
zikatumia nafasi zao katika kuzisimamia ipasavyo haki hizo.
‘Ukizungumza Haki za binadamu unazungumza
kusishi katika mazingira mazuri,Afya,Kuishi,Chakula hivyo ukikivunja kimoja
kinakuplekea katika mazingira mengine kwa hivyto kwa misingi hiyo kuna haja ya
kuimarisha juhudi za pamoja baina ya serikali na wadau wote wa haki za
binadamu’.amesema Mohamed
Hata hivyo Mohamed amesema serikali kwa kushirikiana na taasisi za haki za bindamu ni vyema zikatoa elimu kwa jamii kuhusu kuzifahamu haki zao ili kuweza kukuza na kuendeleza haki hizo.

Post a Comment