NA MUSSA KHALID DAR ES SALAAM
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU
Mkoa wa Ilala jijini Dar es salaam imesisitiza kuendelea kutilia mkazo wa
kudhibiti mianya ya Rushwa kwenye miradi mbalimbali ikiwemo ya
elimu,Maji,Ujenzi na miundombinu katika miezi mitatu ijayo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi leo jijini
Dar es salaam Mkuu wa Takukuru Ilala Christopha Myava amesema lengo lao ni
kudhibiti vitendo vya Rushwa ilikuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa
ufanisi na inakamilika kwa wakati uliopangwa.
Myava amesema watahakikisha miradi yote
inayotekelezwa katika jiji la Dar es salaam wanaifuatili kwa lengo la kuziba
mapema mianya ya Rushwa kabla upotevu wa fedha haujatokea ili iendane na
thamani halisi ya fedha zilizotolewa.
Aidha Mkuu huyo wa TAKUKURU ametoa onyo kwa baadhi
ya wananchi wanaotumia jina la kuwa maafisa wa taasisi hiyo kwa kuwadai watu
pesa, kuwa watachukuliwa hatua kali ili kukomesha vitendo hivyo.
Awali Myava ametoa tahmini ya miezi mitatu
iliyopita April mpaka Juni mwaka huu ambapo,amesema TAKUKURU wameweza kuokoa
Shiling i Mill.123 na elfu 50 ambazo zimedhibitiwa kutoka kwa watuhumiwa
kujipatia fedha hizo kinyume na sheria.
Hata hivyo Mkuu huyo wa TAKUKURU Mkoa wa Ilala
amewataka wananchi wa mkoa huo kuendelea kuonyesha ushirikiano wa taasisi hiyo
kwa kutoa taarifa za vitendo vya Rushwa pindi wanapozibaini katika maeneo yao.

Post a Comment