NA
MUSSA KHALID
Wadau
mbalimbali nchini wametakiwa kujitokeza kutembelea vituo vya makumbusho na
Malikale ili wapate elimu ya kuifahamu asili yao ya masuala ya kale na historia
na kuboresha utalii wa ndani.
Hayo
yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho
ya Taifa Dkt Noel Lwoga wakati akizungumza katika kikao cha baraza la
wafanyakazi wa makumbusho ya Taifa ambacho kimefanyika Mikindani Mkoani Mtwara
kwa lengo la kujadili mpango mkakati wa utekelezaji wa majukumu katika mwaka
2021/2022.
Dkt Lwoga amesema kwa mwaka uliopita wamepata
mafanikio kwa kuongezeka kwa wageni laki moja na elfu arobaini na nne (144,000)
ikiwa ni ongezeko la mwaka uliomalizika hivyo ni chachu kwa watumishi wa
Makumbusho hiyo kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuendelea kuongeza wageni
zaid.
‘Hii ni kama chachu kuona taasisi inaweza
kujitangaza zaidi hivyo ni wakati wakufanya kazi zaidi ili kuyafikia malengo la
Milioni mbili lakini pia kuongeza mapato
kufikia Bill 6 kwa miaka mitano ndani ya Makumbusho ya Taifa’amesema Dkt Lwoga
Aidha Mkurugenzi huyo ametoa wito kwa wadau
kuonyesha uzalendo na kujivunia sifa na utaifa wa urithi wa nchi yao kutokana
na kuwa na vivutio mbalimbali sambamba na kushiriki katika matamasha ambayo
yamekuwa yakiandaliwa na Makumbusho ya Taifa.
Dkt Gwakisa Kamatula ni Mkurugenzi wa Makumbusho ya
Azimio la Arusha amesema kikao hicho kimeongeza hamasa ya utekelezaji wa
majukumu ambayo wamejipangia.
Kwa upande wake Afisa Mipango wa Makumbusho ya Taifa Neema Mbise amesema kikao hicho kimeto mwelekeo wa utekelezaji wa bajeti wa mwaka 2021/2022 lakini kuhamasisha wajumbe kuonyesha uwezo wao katika ufanyaji wa kazi ili kufanikisha malengo waliyojiwekea.

Post a Comment