Msajili wa vyama vya Siasa Nchini Jaji Francis
Mutungi akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es salaam
.....................................................
NA MUSSA KHALID DA ES SALAAM
OFISI ya Msajili wa Vyama vya Siasa inatarajia
kukutana na wadau mbalimbali wa vyama vya Siasa likiwemo Jeshi la Polisi kwa
lengo la kuweka majadiliano ya kuwa na maridhiano kati ya Jeshi hilo pamoja na
vyama vya siasa katika ufanyaji wa shughuli zao.
Msajili wa vyama
vya Siasa Nchini Jaji Francis Mutungi ameeleza hayo leo jijini Dar es salaam
wakati akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake ambapo amesema nia ya
vikao hivyo ni kuweka mazingira rafiki na maelewano baina ya vyama Siasa.
Amesema pindi
alipokutana na wanahabari Tar 6 mwezi Juni kuna baadhi ya watu wamejadili na
kutoa hoja zao hivyo alikutana na Jeshi la Polisi,TCD pamoja na Mwenyekiti wa
baraza kwa lengo la kushauriana ili zoezi hilo liwe na uzito.
Aidha Jaji Mtungi
amesema Septemba 23 mwaka atafanya kikao cha Ofisi ya Msajili na Jeshi la
Polisi kwa lengo la kujadili na kupata ufumbuzi juu ya malalamiko yanayotolewa
na baadhi ya vyama vya Siasa katika ofisi hiyo.
‘Baada ya kamati ya
uongozi kukaa huwa inapanga tarehe ya baraza lenyewe na sio kamati tu ndio
inaamua kupanga bali inaongozwa na kanuni ya baraza la vyama siasa ambapo
kanuni ya 24 ndio inayoeleza kwamba kamati ya uongozi itapanga natehe ya baraza
kwa kutoa notisi siku 14 na kikao hiki kitafanyikia Dar es salaam hivyo tar 13
mwezi wa 10 baraza litakwenda kufanyikia Zanzibar’amesema Jaji Mutungi
Msajili huyo
amesema kikao cha wadau kitaendeshwa bila ya kuepo upendeleo kwani utaendeshwa
na Waziri ambaye hana mafungano ya vyama siasa ili kutia fursa kwa vyama vya
Siasa kuelezea chagamoto zinazowakaba na kufikia Maridhiano.
Ikumbukwe kuwa
vikao hivyo vinakuja ilhali kuwa bado kunamalalamiko ya baadhi ya
wadau wa vyama vya Siasa kushidwa kufanya mikutano yao kwa kueleza Jeshi la
Polisi kuwaingilia.


Post a Comment