Mkuu wa Kitendo cha Masoko wa Kampuni ya World Logistics Company Limited (WLC)Agnes Daniel (kulia) na Afisa Masoko wa (WLC) Apaisaria Godvice (kushoto) wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam (picha na Emannuel Mbatilo)
.....................................................................................
NA MUSSA KHALID
Wakati dunia ikihangaika na janga la UVIKO
19,Kampuni ya World Logistics Company Limited (WLC) imekuja na suluhisho la
kuwasaidia wajasiriamali na wote wanaoagiza bidhaa zao nje ya nchi kupata
bidhaa zao kwa urahisi.
Hayo yamejiri wakati kumekuwepo na changamoto
ya uwepo wa Janga la UVIKO 19 hasa kwa wafanyabiashara ambao ambao hawajachanja
hali ambayo imepelekea kampuni hiyo kushiriki kwa kurahisisha huduma na kulinda
afya za watanzania.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es
salaam,Mkuu wa Kitendo cha Masoko kampuni ya (WLC) Agnes Daniel amesema wameanzisha
huduma iitwayo Cargo Pickup&Delivery Service ili kurahisisha huduma kwa
wafanyabiashara kwa kutafuta mzigo au bidhaa kutoka kiwandani na sehemu
zilipoagizwa kwa kuzisafirisha kuja nchini.
‘Katika sekta yetu hii ya lojistiki na
usafirishaji,wahanga wakubwa ni wafanyabiashara na wajasiriamali wanaoagiza
bishaa zao kutoka nje ya mipaka yetu hivyo tumeona ili ndugu zetu wasiendelee
kuumia tumeamua kuja na suluhisho’amesema Agnes
Kwa upande wake Afisa Masoko wa (WLC)
Apaisaria Godvice amesema wameanzisha huduma hiyo kwani itamsaidia
mfanyabiashara aliyeagiza mzigo kuepuka usumbufu,gharama za safari,hotel na
michakato mingine ambayo itamgharimu pesa pamoja na muda
Hata hivyo imeelezwa kutokana na uzoefu wa
kampuni hiyo kwa miaka 15 wamekuwa wakiwasaidia
wafanyabiashara,wajasiriamali,makampuni na watu binafsi wanaonunua bidhaa nje
ya Tanzania.

Post a Comment