KITS YATANGAZA UJIO WA MAWAKALA WAUTALII ZAIDI YA 30 NCHINI.

Afisa Muendeshaji Mkuu wa Kampuni ya Kimataifa inayojihusisha na masuala ya Utalii Kilimanjaro International Tourism and Safaris (KITS) Francis Malugu (kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Masoko Bodi ya Taifa ya Utalii (TTB) Felix John (katikati) pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya Wellwork Hotel Sameer Ismail (kushoto)

.............................................................

NA MUSSA KHALID DAR ES SALAAM

Takriban mawakala wa utalii zaidi ya 30 kutoka nchini Marekani,Lithuania na Ufaransa wanatarajiwa kuja nchini kwa ziara ya mafunzo ya mazao ya utalii pamoja na matembezi.

Imeelezwa kuwa Mawakala hao  wataingia nchini kuanzia Novemba 23 mwaka huu kufuatia kupata taarifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluh Hassan kushiriki kwenye kutengeneza makala ya Filamu ya Utalii Royal Tour ambapo atakuwa muongozaji mkuu wa zaira hiyo ya kufanya utalii.

Akizungumza jijini Dar es salaam wakati akitambulisha ujio wa watalii hao,Afisa Muendeshaji Mkuu wa Kampuni ya Kimataifa inayojihusisha na masuala ya Utalii Kilimanjaro International Tourism and Safaris (KITS) Francis Malugu amempongeza Rais wa kutangaza Tanzania kwani itasaidia kuongeza nguvu kuvutia utalii na kukuza uwekezaji.

"Mara baada ya kupata taarifa mapema za utengenezaji wa makala hiyo ya filamu na kwamba Rais Samia Suluhu Hassan ndiye atakayekuwa muongozaji mkuu, tuliwataarifu mawakala wa Utalii katika vyama vya utalii duniani ambavyo KITS ni mwanachama wake na zaidi ya mawakala 30 waliomba na kuthibitisha kuja kuitembelea Tanzania, Novemba mwaka huu." Ameesema Malugu.

Aidha amesma matarajio yao kuwa makala hiyo inayorekodiwa na Mh.Rais Samia itakuwa nyenzo muhimu katika shughuli za utangazaji zinazoendelea ili kuisaidia nchi kufikia lengo la watalii millioni 5 na mapato ya dola za kimarekani bilioni 6 ifikapo mwaka 2025 licha ya kuwepo kwa changamoto za Uviko 19 zinayoikabili dunia.

Kaimu Mkurugenzi wa Masoko Bodi ya Taifa ya Utalii (TTB) Felix John amesema ujio wa mawakala hao wa utalii ni fursa muhimu kimkakati katika kuhakikisha wanafikia malengo waliyowekewa ya serikali ifikapo mwaka 2025 nchi iwe na uwezo wa kuvutia watalii wasiopungua Mill 5 na kuliingizia taifa fedha za kigeni.

Sameer Ismail ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Wellwork Hotel amesema wametengeneza Hotel zenye hadhi za kwa lengo la kuwasaidia wageni wanaowasili nchini kupata hifadhi za malazi katika hotel hizo.

Hata hivyo Kampuni ya KITS ambayo Makao Makuu yake yapo nchini Marekani imesema itasaidia Filamu ya Utalii kuonyeshwa kwa mawakala hao ili kuvutia utalii katika nchi ya Tanzania.

0/Post a Comment/Comments