LHRC:MATUKIO YA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO YAONGEZEKA.

Mkurugenzi   mtendaji   wa   Kituo  cha  Sheria  na  Haki  za  binadamu ( LHRC)  Anna  Henga (picha na maktaba).  

..........................................................................

NA SALYM BITCHUKA

Imeelezwa  kuwa  ukatili  dhidi  ya  wanawake  na   Watoto hapa  nchini  umeongezeka  suala  ambalo  linahitaji  ufumbuzi  na  hii  ni   kwa  mujibu  ripoti  ya Haki  za  Binadamu  ya  mwaka  2020 iliyotolewa na  Kituo  cha Sheria  na Haki  za Binadamu  nchini.

Kwa mujibu  wa  ripoti  hiyo  Matukio  ya  ukatili dhidi  ya  Wanawake  yaliyotolewa  na vituo  vya  polisi  nchini  yalikuwa  ni  26,544 ikilinganishwa  na mwaka  2019 ambapo  matukio  yalikuwa  ni 23,685 hii  ikiwa ni  ongezeko  la  asilimia  5.7, Pia vitendo  vya  ukatili  dhidi  ya  watoto  kwa mujibu  wa  taarifa  za  jeshi  la  polisi  viliongezeka.

Hayo   yameelezwa   leo  jijini  Dar  es Salaam  na  mkurugenzi   mtendaji   wa   Kituo  cha  Sheria  na  Haki  za  binadamu ( LHRC)  Anna  Henga  wakati  wa  uzinduzi  wa  mbio  Maalum  za  Haki  Marathon  ikiwa  ni  sehemu  ya  kuelekekea  Maadhimisho  ya  siku  ya  kimataifa   ya  Haki  za  Binadamu  Disemba  kumi  mwaka  huu.

Kwa  upande  wake  mratibu  wa  Haki  Marathon  Deus  Mtukamazina  na  Mkurugenzi  wa Ujengaji  uwezo  na  uwajibikaji  LHRC Felister  mauya  kwa pamoja  wameleelezea  mbio  hizo  za  Haki  Marathon  zimelenga  kuwajengea  uelewa  na kuwawezesha  Watanzania  kutambua  wajibu  wao  wa kulinda  haki  za  Binadamu  nchini.

Mbio  za  haki  Marathon   zitafanyika  kwa  njia  ya  mtandao   kuanzia  Oktoba  17 mwaka  huu  2021  na  kufikia  kilele Desemba  10 2021  ikiwa  ni  sehemu  ya  maadhimisho  ya  siku  ya  Kimataifa  ya Haki  za  Binadamu na zikitarajia kuwa  na washiriki  zaidi  ya 1,000  huku  kauli  mbiu  ya  mbio  hizo  ikiwa  ni  ‘’ HAKI NI MAENDELEO ‘’


 

0/Post a Comment/Comments