MACHINGA DAR WAPINGWA STOP KUFANYA BIASHARA NJIA ZA WATEMBEA KWA MIGUU

 







Asema agizo hilo ni kwa Wafanyabiashara Mkoa mzima.

 

Amtaka DC Ilala na Uongozi wa Machinga kuweka utaratibu mzuri kuwapanga Machinga Kariakoo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Amos Makalla* amepiga marufuku *ufanyaji wa Biashara Kwenye maeneo hifadhi ya barabara* zote za Mkoa huo baada ya utaratibu huo kuwa *chanzo cha uvunjifu wa amani na ongezeko la ajali.*


*RC Makalla* ametoa maelekezo hayo alipotembelea *Soko la Kariakoo* na kujionea Kero ya *Ufanyaji biashara holela Kwenye maeneo ya watembea kwa miguu*.


Kutokana na hilo *RC Makalla* amewaelekeza *Mkuu wa Wilaya ya Ilala* kufanya kikao na Wafanyabiashara hao Jumatatu ya *September 13* na kuainisha maeneo ya kuwapeleka wote waliovamia *hifadhi ya Barabara.*


Aidha *RC Makalla* amewaelekeza Kuangalia utaratibu mzuri wa *kufunga na kufungua baadhi ya Mitaa Kariakoo kwaajili ya kufanya biashara* Kutokana na *ufinyu wa maeneo* ili Waweze kupata riziki.


Hata hivyo *RC Makalla* amesema kwa tathimini aliyofanya amebaini *Hali ya Ufanyaji biashara holela Dar es salaam ipo kwa kiwango kikubwa na kuwanyima watembea miguu haki zao za msingi.*


Pamoja na hayo *RC Makalla* ameelekeza Manispaa zote za Mkoa huo kuweka *Vibao vya kuzuia biashara Kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.*

0/Post a Comment/Comments