NDOMBA-DORAN ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MTENDAJI & AFISA MTENDAJI MKUU ATE




Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) wametangaza rasmi kumteua Bi. Suzanne Ndomba-Doran kuwa Mkurugenzi Mtendaji & Afisa Mtendaji Mkuu wake akichukua nafasi ya Dkt. Aggrey Mlimuka ambaye amestaafu.


Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya ATE Bi. Jayne Nyimbo -Taylor inasema kwamba Bi. Ndomba -Doran ataanza rasmi kutumikia nafasi yake hio mpya mnamo Oktoba 1 mwaka huu. 


Kabla ya kushika nafasi hii alikua ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji na Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa ATE.

0/Post a Comment/Comments