NEMC YAENDELEA KUSISITIZA WAWEKEZAJI KUZINGATIA USALAMA WA WANANCHI.

Mkurugenzi Mkuu wa baraza hilo Dkt Samueli Gwamaka

...........................

Baraza  la Taifa la uhifadhi na usimamizi wa  mazingira –NEMC limewataka wamiliki wa vituo vya mafuta pamoja na wanaohitaji kufanya uwekezaji huo kuzingatia usalama wa wananchi ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wananchi wa eneo husika ili kuondoa kero na migogoro isiyofaa pamoja na kuhatarisha maisha yao.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Mkurugenzi Mkuu wa baraza hilo Dkt Samueli Gwamaka amesema hatari hizo ni pamoja na vituo hivyo kushika moto ambapo ameongeza kuwa muwekezaji yoyote atakayekiuka sheria hizo atachukuliwa hatua za kisheria.

Amesema  kumekuwa na ombwe la muingiliano wa shughuli inayotokana na miradi hiyo huku akitoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano pale ambapo wanaona mradi unaanzishwa bila kufuata sheria.

Sambamba na hilo Dkt Gwamaka amewataka wawekezaji wote ambao bado hawajasajili miradi yao kuanza kusajili miradi yao katika baraza hilo ili kuepuka faini.

Mwenyekiti serikali ya mtaa wa Goba Mustafa Mponda amekiri uwepo wa changamoto za kupata ya kupata ushirikiano kutoka kwa wamiliki wa vituo hivyo hasa katika miradi ya maendeleo kama vile shule.

Kwa upande wao baadhi  wananchi wa mtaa wa Goba wamesema kuwa licha ya ujenzi wa vituo hivyo lakini swala utoaji wa elimu juu ya kujikinga na madhara ya ujenzi wa vituo hivyo haitolewi.

Hivi karibuni Baraza la Taifa la uhifadhi na usimamizi wa mazingira –NEMC limezitoza faini ya shilingi bilioni 5.1 kampuni za uuzaji na usambazaji wa mafuta kwa kushindwa kufanya tathmini ya athari kwa mazingira –TAM.

0/Post a Comment/Comments