.....................................................................
NA
MUSSA KHALID
Serikali
imesema inaendelea kuboresha vituo mbalimbali vya Afya nchini pamoja na Shule
ili kusaidia watanzania kupata huduma kwa ukaribu.
Kauli hiyo
imetolewa leo jijini Dar es salaam na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ofisi ya Rais
Tawala za mikoa Na Serikali za Mitaa TAMISEMI Kitengo cha Afya Dkt.Grace
Magembe katika hafla ya Ufungaji rasmi wa Mkutano wa Kitaifa wa mradi wa USAID
Kizazi Kipya.
Dkt Magembe
amesema tayari Rais Samia ametenga Bill 37.5 ambazo zimepelekwa kwenye tarafa
takriban 220 kwa ajili ya kujenga vituo vya Afya huku msukumo ukiwekwa kwenye
mradi unaofuata watu kujiunga katika mifuko ya bima ya Afya.
Kwa upande
wake Mkurugenzi wa Shirika la PACT Tanzania Mariana Balampama amesema
wataendelea kushirikiana na serikali kuangalia Afua mbalimbali kwani katika
miaka 5 wamefanya kazi katika Halmashauri zaidi ya 150 Tanzania Bara pamoja na
Zanzibar.
Ananthy
Thambinayagam ni Mkurugenzi wa Ofisi ya Afya kutoka Shirika la USAID nchini
Tanzania amesema lengo la mradi huo wa Kizazi Kipya ni kuwasaidia vijana
kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya Virusi vya Ukimwi.
Hata hivyo imeelezwa kuwa kupitia mradi huo wa Kizazi Kipya vijana zaidi ya 9000 wameweza kupatiwa ufadhili wa kusoma mafunzo ya ufundi stadi na kupatiwa vifaa vya kuanzisha biashara sambamba na kuungwanishwa na vikundi vya kuweka na kukopa ili kuongeza biashara zao.

Post a Comment