WANANCHI KATA YA KEKO DAR WALALAMA KWA MADAI YA KAMPUNI YA REDSEA CO.LTD KUTOFATA TARATIBU ZA UJENGAJI WA MFEREJI WA MAJI MACHAFU.

    

Wananchi wa Kata ya Keko Manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam wakiwa wamesimama nje ya geti la Kampuni ya REDSEA CO.LTD ili kupata muafaka wa mgogoro wamfereji wa maji unaopita katika maeneo yao

Mbunge wa Jimbo la Temeke Dorothy Kilave alipokuwa akishuhudia mfereji huo 

Mfereji wa maji machafu unaodwaiwa kuzibwa na Kampuni ya REDSEA CO.LTD na kusababisha kukumbwa na mafuriko ya maji machafu

Diwani wa Kata ya Keko Jasdeep Singh Babhra akizungumza na mwandishi wa habari hizi

.................................................................

NA MUSSA KHALID ,DAR ES SALAAM

Wananchi wa Kata ya Keko Manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam wameilalamikia serikali kwa kutowatatulia changamoto ya mfereji wa maji ambao unadaiwa kuzibwa na Kampuni ya REDSEA CO.LTD na kusababisha kukumbwa na mafuriko ya maji machafu.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi leo jijini Dar es salaam wananchi hao ambao wamejikusanya pembezoni mwa kampuni hiyo na kutoa kero zao mbele ya Mbunge wa Jimbo la Temeke Dorothy Kilave wamesema kutokana na kutoboreshwa kwa mfereji huo ambao umejengwa eneo la Azania umesababisha wakumbane na adha hasa nyakati za mvua.

Wamesema ujenzi wa mfereji huo umeanza kujengwa kwa muda mrefu na haujawekwa mwendelezo wa maji  kwenda baharini hivyo kusababisha kujaa maji  na kuingia katika makazi ya watu.

Akizungumzia Changamoto hiyo Mbunge wa Jimbo la Temeke Dorothy Kilave amesema baada ya kukutana na Uongozi wa Kampuni hiyo wameazimia kupewa maelezo ya kibali cha kujenga mfereji huo ambacho wamepewa na Manispaa kama wanavyodai ili waweze kupitia na kisha kuchukua hatua.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TARURA Temeke Mhandisi Kweyamba Adelhard amesema watafanya upembuzi wa kibali ambacho kampuni hiyo imeomba cha kujenga mfereji huo na kama imekiuka masharti watamrudisha Manispaa na kukifuta kibali hicho.

Naye Diwani wa Kata ya Keko Jasdeep Singh Babhra amesema wanaendelea kufuatilia na hivyo amewataka wananchi kuwa watulivu kwani yeye ni mwakilishi wao hivyo atahakikisha linatatulika.

Diwani huo amesema Mfereji huo sio wa Wilaya bali ni waKitaifa hivyo baada ya kufika kwa Mbunge pia atalifikisha Mpaka kwa waziri wa Ujenzi pamoja na TAMISEMI ili changamoto hiyo iweze kutatulika .

0/Post a Comment/Comments