ZAHANATI ILIYO NA MUHUDUMU MMOJA HUKU IKITOA HUDUMA KWA ZAIDI YA WAKAZI ELFU NANE..

Muhudumu  Pekee  Wa  Zahanati  Ya  Nambunju  Rehema  Saidi  Mhimbwa  

Baadhi  Ya  Wakazi Wa Nambunju Wakikagua Kituo  Cahoa Cha Afya

..............................................................................................

 NA SALIM  BITCHUKA

Wakazi  wa  kijiji cha  Nambunju Kata  Mbwara  tarafa  ya  Mohoro  wilaya ya  Rufiji   mkoani  Pwani   wameiomba  Serikali  kuwaongezea  Wahudumu  wa  Afya  Katika  Zahanati  iliyopo  kijijini  hapo.

Wakizungumza  na  kituo  hiki kutoka  mkoani  Pwani  wakazi  hao  wamesema  katika  Zahanati  hiyo  kumekuwa  ma  muhudumu  mmoja  kitendo  kinachopelekea  kukosekana  ufanisi  wa  kazi  na  kuhatarisha  maisha  ya   wakazi  wa  kijiji  cha  Nambunju   hasa pale  kunapokuwepo  wagonjwa  wengi  kwa  wakati  mmoja  katika  kituo  hicho  cha  Afya.

Aidha  kwa  upande  wake  muhudumu  pekee  wa  Zahanati  ya  Nambunju  Rehema  Saidi  Mhimbwa   amekiri  kuwa  ni  yeye  pekee  anayehudumia  katika  kituo  hicho  kwa  zaidi  ya miezi  ya  miezi  Mitano huku  akisema  kuwa  changamoto  kubwa  ni  wingi  wa watu  wanaohitaji  huduma  na  pale  anapopatwa  na  dharura  hupelekea  kufunga  kituo.

Mbali  na  uhaba wa  watoa  huduma  katika  kituo  hicho   cha  Afya , kijiji  cha  Nambunju  Mkoani  Pwani  kinakabiliwa  na  kero  nyingi  ikiwemo  ubovu   wa  barabara , ukosefu  wa  usafiri  wa  kutosha , ukosefu  wa  Maji  safi  na Salama , vyumba  vya   madarasa ,madawati, ukosefu  wa  mawasiliano  ya  simu ya   uhakika kitendo   kinachowaibua   wananchi  kutaka  viongozi  wa ngazi  za  juu  wa  Serikali  kutembelea  Kijijini  hapo.

Kwa  upande  wake  Afisa  Mtendaji  wa  Kijiji  cha  Nambunju   Maliki  Hamidi  pamoja  na  Mwenyekiti  wa  Kijiji  Abdallah  Hemedi  Kipuli  kwa  pamoja  wamekiri  uwepo  wa matatizo  hayo  huku   wakisema  kuwa  baadhi  ya  matatizo  tayari   yamewasilishwa  katika  ngazi  husika  ikiwemo  ubovu   wa  barabara pamoja  uhaba   wa  watoa  huduma   katika  Zahanati  ya  Nambunju.

Kijiji  cha  Nambunju  Kilichpo  Wilaya  ya  Rufiji  Mkoani  Pwani  kina vitongoji  vitano  huku  kikiwa  na  wakazi   zaidi  ya  elfu   nane  ambao  shughuli  yao  kubwa  ni  kilimo 


 

0/Post a Comment/Comments