FULL STORY, OMMY DIMPOZI KUUGUZWA NA ALIKIBA




Na Mwandishi wetu, 

Msanii wa Bongo Fleva, Omary Nyembo, ‘Ommy Dimpoz’, amefunguka jinsi Alikiba alivyomsaidia kwenye maisha yake ikiwamo kumuuguza.


Akizungumza wakati wa Listening Party ya Albam ya Mfalme wa Bongo Fleva, AliKiba ya ‘Only one King’ usiku wa kuamkia leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Ommy Dimpoz amefunguka kuwa mbali na kushirikiana kwenye wimbo ya NAINAI kuna mambo mengine mengi ambauyo watu hawayajui.


“Ukiacha na historia yetu ya wimbo wa Nai nai iliyonitoa kwenye gemu, wakati napitia matatizo ya kiafya tulikuwa hapa Serena kwenye kamati ya harusi yake tukatoka tukaenda kula sehemu baada ya kula chakula kilinikwama.


“Kilivyonikwama tulikuwa na Alikiba na Gavana Ali Hassan Joho wa Mombasa, Ali aliingiwa na huzuni alipoona napata shida kula akasema tutafanyaje akamwambia Gavana najua unamadokta wazuri sana Kenya nanaona ndugu yangu anateseka kweli hata hii harusi yenyewe hana hata raha nayo,”amesema Ommy Dimpoz.

0/Post a Comment/Comments