HALOTEL YASHEHEREKEA MIAKA 6 KWA KUTOA MSAADA KWA WATOTO WENYE MATAIZO YA KIAFYA (MOI).

Naibu Mkurungenzi wa Halopesa Magesa Wandwi,Afisa Mahusinao ya nje Yassir Matsawily (katikati) wakiwa pamoja na Mkuu wa kitengo cha Bidhaa na Masoko Sakina Makabu (wa kwanza kulia)  na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo wakikabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ya Kijamii  kwa  Afisa mahusiano wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili  Patric Mvungi ( wa pili kulia) na baadhi wa wauguzi leo wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipowatembelea watoto walioko katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) na kuwapelekea mahitaji hayo ikiwa ni katika kuadhimisha miaka sita ya utoaji wa huduma za mawasiliano hapa nchini.

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Mawasiliano Halotel Pamoja na baadhi wa maofisa wa wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakikabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ya kijamii leo wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipowatembelea watoto walioko katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) na kuwapelekea mahitaji hayo ikiwa ni katika kuadhimisha miaka sita ya utoaji wa huduma za mawasiliano hapa nchini.

Mkuu wa kitengo cha Bidhaa na Masoko Sakina Makabu akiongea na waandishi wa habari leo, baada ya kukabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ya kijamii kwa watoto na wazazi walioko katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipowatembelea na kuwapelekea mahitaji hayo ikiwa ni katika kuadhimisha miaka sita ya utoaji wa huduma za mawasiliano hapa nchini.


Afisa Mahusiano ya nje wa Halotel Yassir Matsawily akiongea na waandishi wa habari leo, baada ya kukabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ya kijamii  kwa watoto na wazazi walioko katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili  wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipowatembelea na kuwapelekea mahitaji hayo ikiwa ni katika kuadhimisha miaka sita ya utoaji wa huduma za mawasiliano hapa nchini.

Mmoja wa wazazi Rose Vincent katika Taasisi ya Tiba na Mifupa Muhimbili (MOI) akitoa shukrani kwa Wafanyakazi wa Kampuni ya Halotel kwa kuwakumbuka na kuwaletea mahitaji mbalimbali ya muhimu ya kijamii abayo yata wasadia sana pindi wanapopata matibabu hospitalini hapo.

....................................................................

NA MUSSA KHALID,DAR ES SALAAM

Katika kuonyesha thamani na kujali jamii kwenye Sekta ya Afya na elimu,Kampuni ya simu ya Halotel imetoa mahitaji muhimu kwa watoto wenye changamoto ya kiafya ya vichwa vikubwa na mgongo wazi waliolazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) yatakayowawezesha kuimarisha afya zao.

Hayo yamejiri leo jijini Dar es salaam katika kuadhimisha miaka 6 ya kampuni hiyo na utoaji wa huduma ya mawasiliano ambapo wameadhimisha kwa kwa utoajni wa Dawa muhimu ya kibinadamu ili kuwasaidia afya zao pindi wawapo wodini wakisubiri kupatiwa matibabu kwa njia ya upasuaji.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mahitaji hao,Afisa Uhusiano wa Nje Halotel Yassir Matsawily amesema katika kuhakikisha wanasaidia sekta afya wametumai fursa hiyo kuwatembelea watoto hao kwa kusheherekea na kuwapa misaada ili waweze kuimarika kiafya.

‘Hii imekuwa kawaida yetu kwa kutoa kidogo tulichojaaliwa  kwa wnzetu katiika jamii kwani lengo letu ni kuonyesha upendo kwao na kutambua thamani yao katika jamii ya watanzania’amesema Yassir

Kwa upande wake Msemaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) Patrick Mvungi ameipongeza Kampuni hiyo kwa kuguswa na kutoa msaada wao kwa jamii huku akiyataka makampuni mengine kuiga mfano kwani wanawasaidia wagonjwa kupata faraja.

‘Hii ni hatua mpya na kubwa kwani imekuwa endelevu kwetu sisi katika kuimarisha ushirikiano wetu na Halotel kwa kiwango cha juu hasa katika kuboresha sekta ya afya kwa ujumla’amesema Mvungi

Mmoja wa wazazi Bi Rose Vincent akizungumza kwa niaba ya wazazi wenzake baada ya kukabidhiwa msaada huo wameiomba Kampuni hiyo kuendelea kuwa kuonyesha mchango wao kwa jamii kwani wanawasaidia watanzania wote wenye uhitaji walio katika vituo vya afya.

Hata hivyo Kampuni hiyo imesema huo ni muendelezo wa kuendelea kutoa mchango wao kwa jamii ili kuunga mkono juhudi za Rais Samia katika kuboresha huduma za afya.

0/Post a Comment/Comments