Waandamanaji waliandamana
katika mji mkuu wa sudan na kote nchini humo
Wanajeshi wamevamia nyumbani kwa
mshauri wa habari wa Waziri Mkuu wa Sudan Abdalla Hamdok na kumkamata mapema
leo.
Televisheni ya Al hadath imesema
wanajeshi wa Sudan wasiotambulika waliwakamata mawaziri wanne wa serikali na
raia mmoja mwanachama wa baraza kuu la serikali.
Duru zinasema kuwa Waziri Mkuu
Abdalla Hamdok amewekwa chini ya kifungo cha nyumbani.
Haya
yalijiri siku moja tu baada ya Mjumbe Maalum wa Marekani kwa Pembe wa
Afrika Jeffrey Feltman kukutana na viongozi wa kijeshi na kiraia mjini Khartoum
kutafuta mwafaka katika mzozo huo.
Source:DW
Post a Comment