SAU YAMPONGEZA RAIS SAMIA KUFANIKISHA UPATIKANAJI WA MKOPO WA TSH TRIL.1.3 KUTOKA IMF

Katibu Mkuu Chama Cha SAU Majalio  Kyara.

TAARIFA KWA UMMA

YAH; UZINDUZI WA KAMPENI YA MAENDELEO KWA USTAWI WA TAIFA NA MAPAMBANO DHIDI YA UVIKO-19

Chama cha sauti ya umma(SAU) tuna mpongeza Mhe.Rais SAMIA SULUHU HASSAN, Waziri Mkuu na Kamati nzima iliyoshiriki katika kufanikisha upatikanaji wa mkopo huu wa Tsh 1.3trillion kutoka IMF na kutengeneza matumizi sahihi, ya kiubunifu na bora zaidi kwa pesa hizi.

Pesa hizi pamoja na kwenda kusaidi kupunguza/kuondoa maambukizi ya uviko-19, pia zitaleta maendeleo kwa nchi na jamii yetu kwa kuleta AJIRA nyingi, elimu bora,Maji,huduma bora za afya n.k 

Aidha tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuruhusu matumizi ya manunuzi ya SINGLE SOURCE kwa fedha hizi.Hii itasaidia miradi iliyokusudiwa kukamilika ndani ya muda unaotakiwa 

Niwaombe Viongozi na Watanzania wote tutoe ushirikiano mzuri katika kampeni hii na kuweka maslahi ya Taifa kwanza na kwa uaminifu 

Imetolewa  na:

Majalio Kyara

Katibu Mkuu Chama Cha 

SAU

0/Post a Comment/Comments