SEMINA YA UNABII YA KITABU CHA UFUNUO.



Takribani wachungaji 89 na waumini 201 walihudhuria semina hiyo huko kigamboni na kwa njia ya mtandao wa youtube Pamoja na zoom,

......................................................................

Kanisa la shincheonji church of Jesus nchini Tanzania, limeandaa semina ya kitabu cha ufunuo kwa ajili ya wachungaji na watumishi wa Mungu wa Tanzania. 

Semina hiyo ilifanyika Mnamo terehe 15 na tarehe 16 mwezi Oktoba, huko kibada kigamboni kaitaka kanisa la Presbyterian na pia kwa njia ya mtandao wa zoom na youtube. 

Takribani wachungaji 89 na waumini 201 walihudhuria semina hiyo huko kigamboni na kwa njia ya mtandao wa youtube Pamoja na zoom, na kufanya jumla ya watu waliozudhuria semina ya ntarehe 15/10 kuwa 290 na pia jumla ya watu walioudhuria tereh 16/10 walikuwa wachungaji 94 na waumini 194 na kufanya jumla wa watu 288. 

Mwenyekiti wa kanisa la shincheonji church of Jesus, Lee Man Hee ambaye ndio alikuwa muhadhiri wa semina hiyo alisema “jukumu langu ni kufundisha na kushuhudia kitabu cha ufunuo , ambacho nimeona na kusikia, ndio mimi mjumbe niliyetumwa kwa makanisa kushuhudia unabii wa kitabu hiki cha ufunuo.” 

Mbali na semina hiyo shincheonji church of Jesus, itaendeleza mafunzo ya semina ya kitabu cha ufunuo kwa muda wa siku 22, kuanzia tarehe 18/10 mpaka tarehe 24/12 kwa njia ya youtube chaneli ya kanisa hilo. 

Wachungaji walioudhuria walivutiwa sana na semina hiyo na kukubali kusign hati ya MOU (memorandum of understanding), hati inayohusu makubaliano yasiyo ya kisheria kati ya makanisa yao na kasina la shincheonji church of Jesus katika kueneza mafundisho hayo ya kitabu cha ufunuo. 

“Makanisa machache yanaweza kufundisha vitabu vya unabii kama vile kitabu cha Daniel na kitabu cha ufunuo japokuwa ndio vitabu muhimu sana kwa sababu vinaongelewa nyakati tulizo sasa ambazo ni nyakati za mwisho, kwa hiyo na mshukuru sana mwenyekiti Lee Man Hee kwakugundua huitaji wa watu kutaka kujua mafundisho ya kitabu cha ufunuo, hii inamaanisha kuwa kuna kitu Mungu amempa ili aweze kuwapa watu wa kigamboni na Dar es saam kwa ujumla”alisema mchungaji Martin Antony Ndoyela kutoka kanisa la EAGT Kisarawe. 

Dr.Nicolous Baibuka ambaye ni mwenyekiti wa umoja wa makanisa ya Pentecost kigamboni alisema “kitabu cha ufunuo ni muhimu sana ni neema kubwa sana kujua kitabu hiki, ndio maana nilivyosikia kuwa mtumishi wa Mungu atafundisha nilitaka kujua Zaidi, mwenyekiti lee man hee alisema hajawah kwenda chou lakini alivyokuwa anafundisha niligundua vyote ni kama biblia inavyosema, nimepata neema kubwa sana kisikia ufunuo. 

0/Post a Comment/Comments