TANZANIA YATARAJI KUWA MWENYEJI ONYESHO LA KWANZA LA UTALII EAC.

Waziri wa Maliasili na Utalii nchini Dkt Damas Ndumbaro(kulia) wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam

.................................................................

NA MUSSA KHALID,

Serikali imesema inaendelea kuimarisha na kukuza sekta ya utalii ikiwa ni pamoja na kuunga mkono juhudi za kutangaza utalii huo nchini ili kuweza kuwavutia wageni kutoka maeneo mbalimbali Duniani.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Maliasili na Utalii nchini Dkt Damas Ndumbaro wakati akizungumza na waandishi wa habari akitoa aarifa ya Tanzania kutajwa kuwa mwenyeji wa Onyesho la Kwanza la Utalii katika nchi za Afrika Mashariki linalotarajiwa kufanyika  tar 9 - 16 mwezi huu jijini Arusha.

Waziri Dkt Ndubaro amesema katika kuunga mkono Royal Tour ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluh Hassan ameianzisha Wizara hiyo imefuta tozo za utalii kwa muda wa wiki moja kwa wale waliojisajili ili tamasha hilo lipewe heshima inayostahili.

Aidha Waziri Dkt Ndumbaro amesema kutokana na nchi ya Tanzania kuandaa onyesho hilo ni heshima kwa nchi kwani litakuwa na manufaa makubwa kwani itasaidia kutangaza vivutio mbalimbali vilivyopo hapa nchini.

Hata hivyo amewataka watanzania wakiwemo Waongoza Utalii pamoja na Vyama vyote wa Utalii nchini kuweza kutumia fursa hiyo kushiriki katika tukio hilo muhimu ambalo kwa mara ya kwanza linafanyika nchini Tanzania.

0/Post a Comment/Comments