SALIM BITCHUKA
Chama cha Wananchi ( CUF)
Kupitia Baraza kuu la Uongozi la Taifa
la chama hicho limewavua uanachama
waliokuwa wanachama wao saba kwa kosa
la kula njama ya kukihujumu chama
kifutiwe usajili .
Akiwasilisha taarifa hiyo
leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa habari,
uenezi na mahusiano na umma Injinia Mohamed
Ngulangwa amesema mbali na kusimamishwa
kwa wanachama hao Baraza kuu
taifa CUF Pia limewasimamisha
uachama wanachama watatu na wanne kupewa
karipio kali la Maandishi.
Injinia Ngulangwa amesema
pamoja na ukweli kwamba kila mmoja
alikuwa na mashitaka yake asilimia 50
ya viongozi hao walishirkiana kula njama
ya kukihu jumu chama.
Aidha Mohammed Ngulangwa
amewataja waliovuliwa uanachama ni pamoja na
aliyekuwa mjumbe wa Baraza kuu la Uongozi
kanda ya Pwani Abdalla Juma Kambaya,
Mkurugenzi wa Mipango na uchaguzi Mohamed
Vuai Makame, Alli Makame Issa na Chande Jidawi.
Wengine waliovuliwa uanachama ni
pamoja na Hamida Abdallah Huweishil,
Dhifaa Mohammed Bakari na Mtumwa Ambar
Abdallah.
Maazimi hayo yamepitishwa na Baraza kuu la Uongozi la Taifa la chama cha Wananchi CUF walipoketi Novemba 5 na 6 mwaka huu 2021 huku likijadili masuala mbali mbali pamoja na kumthibibitisha Mbarouk Seif Salim kuwa mjumbe wa Baraza kuu,na pia Baraza limempitisha kuwa Naibu Katibu mkuu Zanzibar huku Mwadini Jecha akiteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi.
Post a Comment