Timu ya Uganda imeshinda goli mmoja dhidi ya wenyeji Tanzania leo Novemba 29, 2021 kwenye mashindano yanayoendelea ya Afrika ya soka kwa wenye ulemavu CANAF 2021 katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam.
Goli la ushindi la Uganda limefungwa dakika ya 20 kipindi cha kwanza na mshambuliaji Ssempija Julius baada ya kuwahadaa mabeki wa Timu ya Tembo ya Tanzania.
Katika mchezo wa kwanza Tanzania iliibamiza timu ya Morocco 2-1. Wakati Uganda katika mchezo wake na Sierra Leon walifungwa 3-0.
Mchezo huu umechezeshwa na Luciano Antonio kutoka Angola, Mohamed Mwadini kutoka Zanzibar na David Mng'ong'o kutoka Tanzania.
Mechi nyingine zinazochezwa leo ni Sierra Leon na Morroco, Kenya na Zanzibar, Liberia na Gambia pia Nigeria na Misri
Post a Comment