JWTZ YAWATAKA WATANZANIA KUWAEPUKA MATAPELI

Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi hilo,Luteni Kanali Gaudentius Gervas Ilonda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.

...............................

NA MUSSA KHALID.

Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) limewataka watanzania kuwaepuka na wasidanganyike na baadhi ya watu wanaofanya utapeli na kuwalagha vijana kuwa wanawaandikisha kujiunga na Jeshi la kujenga Taifa.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi hilo,Luteni Kanali Gaudentius Gervas Ilonda wakati akitolea ufafanuzi kufuatia kuibuka kwa mwenendo wa baadhi ya watu wakitumia fursa ya uandikishwaji wa vijana kujinufaisha.

Luteni Kanali Ilonda amesema udanganyifu huo unaofanyika umesababisha kuleta usumbufu kwa wananchi wenye vijana wao waliokuwa kwenye Makambi ya Kujenga Taifa jambo ambalo ni kinyume na taratibu.

Aidha Luteni Kanali Ilonda amesisitiza kuwa hakuna nafasi ya kuingia Jeshini kwa kutumia mgongo wa fedha hivyo ametoa rai wa watu wanaohusika katika kuwalangai wananchi kuacha mara moja.

Amewata watanzania kuzifahamu taratibu mbalimbali za kujiunga na jeshi kuwa ni pamoja na kuwa raia wa Tanzani,Umri wa miaka 18-28,kuwa na afya njema ya mwili na akili lakini pia awe hajapatikana na hatia ya makosa yeyote ya jinai,awe na cheti cha kuzaliwa pamoja na cha taalum.

0/Post a Comment/Comments