.......................
NA MUSSA KHALID
Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais
Muungano na Mazingira Hamad Chande amewataka mabalozi wa mazingira nchini kuhakikisha
wanasaidia kudhibiti uharibifu wa mazingira ili vizazi vijavyo viweze kukuta
nchi ikiwa na mazingira mazuri.
Kauli hiyo ameitoa leo wakati akifungua warsha ambayo
imewakutanisha mabalozi wa mazingira kuhusu utekelezaji wa kampeni kabambe ya Hifadhi na usafi wa mazingira inayofanyika
kwa siku mbili jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri Chande amesema kuwa serikali
imewaamini na kuwapa ubalozi ili kusaidia jamii kuweza kuishi kwa amani bila ya
taharuki inayosababishwa na uharibifu wa mazingira.
‘Niwapongeze sana wataalamu wetu kwa
kuwatafuta watu wakawaweka mabalozi kwani bila kujisimamia wenyewe hatotoka mtu
nje ya nchi aje asimamie mazingira yetu bali tunayasimamia wenyewe’amesema
Naibu waziri Chande
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Balozi wa Mazingira
nchini Tanzania,Shekh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Alhad Mussa Salum amewakumbusha
watanzania kuwa utunzaji wa mazingira ni jambo la ibara kwani kufanya uharibu
ni hatari kwa binadamu na viumbe wote.
Kwa upande wake Balozi wa
Mazingira na Kinara wa Umoja wa Mataifa
katika malengo ya maendeleo endelevu Mwanamuziki Bernard Paul, maarufu kama Ben Pol ambaye Juni 6 mwaka huu aliteuliwa na
Waziri Jaffo kuwa balozi wa mazingira amesema itawasaidia kupambana na kutoa elimu kwa jamii juu ya
athari za uchafuzi wa mazingira.
Warsha hiyo imehudhuriwa na mabalozi na wadau mbalimbali wa mazingira nchini wakiwemo wabunge kwa lengo la kufanya uwasilisho kuhusu mpango kazi wa utekelezaji wa kampeni ya uhifadhi wa usafi wa mazingira.
Post a Comment